Monday, April 11, 2016

HOSPITALI IRINGA YAAMRIWA KUPATA UFUMBUZI UTEKETEZAJI TAKA NGUMU

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO



NAIBU Waziri Ofisi ya Makamu wa Raisi Muungano na Mazingira,Luhaga Mpina, ameugiza uongozi wa Hospitali ya Rufaa, Mkoani Iringa kulipatia ufumbuzi haraka suala la uteketezaji wa taka ngumu katika hospitali hiyo.

Mpina alitoa agizo hilo jana alipotembelea Hosptali ya Rufaa ya Mkoa  wa Iringa,ikiwa ni ziara yake ya kukagua usafi wa mazingira na utekelezaji wa sheria ya usimamizi wa mazingira katika viwanda, viliyopo katika mkoa wa Iringa.

Awali ilifahamika kwamba uteketezaji wa taka hatarishi katika hosptali hiyo ya mkoa,umekumbana na changamoto nyingi ikiwa ni pamoja na kuharibika kwa kifaa cha kuteketeza taka hospitalini hapo kwa muda mrefu,pasipo kuwepo jitihada za matengenezo ama taratibu za utekelezaji manunuzi serikalini.

Kwa Upande wake Mganga Mkuu Mfawidhi wa hospital hiyo, dkt Robert Salim,alimueleza Naibu waziri huyo kuwa taka zizalishwazo katika hosptali hiyo zimekuwa zikitupwa katika Dampo la mkoani hapo.

Dkt.Salim alisema kuwa hosptali hiyo imekuwa na wakati mgumu sana katika kuteketeza taka hatarishi kama vile za sindano, gloves, nyembe na bandeji maana haziozi ardhini kirahisi,kutokana na kuharibikiwa na kifaa cha kuteketeza taka hizo.

Akitolea ufafanunuzi sualala za uteketezaji wa taka hatarishi hospitalini hapo, mratibu wa kanda ya nyanda za juu kusini wa Baraza la Taifa la Usimamizi wa Mazingira (NEMC) bw. Godlove Mwamsojo,alieleza kuwa baraza limewahi kutoa ushauri kwa uongozi wa hosptali hiyo kuteketeza taka hizo kwa kusaidiwa na kiwanda cha mbao cha Sao hill kilichopo wilayani Mufindi kwa kuwa kiwanda hicho kina vifaa vya kutosha.

Hata hivyo ushauri huo haukuleta tija sana kutokana na  kwamba hospital hiyo huzalisha taka nyingi,hivyo  kuzidi uwezo wa kiwanda cha Sao Hill kusaidia kuziharibu.

Wakati huo huo, Naibu Waziri Mpina alikagua mazingira ya soko la Mjini Iringa na kushiriki katika usafi wa mazingira pamoja na kupanda miti, ambapo   alipanda mti katika kata ya Kitwivu na kuwaasa wakazi wa Iringa kuwa walinzi wa misitu na kutoa taarifa za wizi na uhujumu wa magogo ili sheria ichukue mkondo wake.

Aidha aliwaasa watunze vyanzo vya maji kama walivyotunza vizuri chanzo cha maji ya chemchem cha Kitwivu,huku akisisitiza umuhimu wa jamii kupanda miti ili kuepuka changamoto za mabadiliko ya tabia nchi.

Naibu Waziri huyo aliiongeza Wilaya ya Mufindi kwa kupitiliza lengo la kupanda miti milioni moja na laki tano kila mwaka katika kila wilaya na kupanda miti milioni thelathini na tano kwa mwaka.

KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI