Sunday, March 6, 2016

WAZAZI WANAOZESHA WANAFUNZI SASA KUKIONA

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO



SERIKALI imepiga marufuku kwa wazazi kuozesha wanafunzi wa kike kwa nia ya kupata ng’ombe na kwamba kuanzia sasa, Ofisa Mtendaji wa Kijiji au wa Kata ambako itagundulika kuwa msichana ameozeshwa au kupata mimba ataswekwa ndani na kufungwa jela.

Hayo yalisemwa juzi na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa,wakati akiweka jiwe la Msingi la vyumba vitatu vya maabara katika Shula ya Sekondari Budalabujiga wilayani Itilima,mkoani Simiyu,kwa kutoa onyo kwa wazazi na walezi wenye kuozesha wanafunzi, hawataachwa na mkono wa sheria.

Majaliwa alisema Serikali haina mzaha katika suala la elimu na kwamba   imedhamiria kuhakikisha kila mtoto anapata elimu hivyo ni jukumu la maofisa hao kuhakikisha wasichana wanasoma hadi kufikia ngazi ya chuo kikuu na zaidi.

“Nasikia hapa Itilima wazazi wanawaozesha watoto wao ili kupata ng’ombe…jambo hili ni marufuku. Mtoto wa kike anapoanza chekechea tunataka amalize hadi chuo kikuu. Acheni kabisa mambo haya (ya kuozesha).” Alisema Waziri Mkuu na kuongeza:

“Kwenye eneo hili hatuna mzaha. Watendaji wa kata na vijiji ambao eneo lao wanafunzi watapata ujauzito, unajua na hukuchukua hatua, na wewe tunakutia ndani na tunakufunga.”  

Waziri Mkuu alisema watendaji hao wanapaswa kushirikiana na walimu wakuu na wakuu wa shule kuhakikisha kuwa wasichana wanakuwa salama.

“Lakini wazazi na walezi nao hatutawaacha, wanaokatisha masomo wanafunzi watachukuliwa hatua. Hatuwezi kuona wasichana wakikatizwa masomo kwa sababu zinazoweza kuzuilika,” alisisitiza.

Kwa mujibu wa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Itilima, John Lyimo, gharama za ujenzi wa maabara hizo tatu za Kemia, Fizikia na Baolojia ni Sh 233,338,000 na tayari zimetumika Sh 180,954,400 zilizotoka halmashauri, wananchi na nguvu kazi pamoja na wadau wa elimu.

KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI