![]() |
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Hamis Kigwangala |
JESHI la Polisi wilaya ya Kahama Mkoani Shinyanga,linamshikilia kwa uchunguzi mtumishi mmoja katika
Hospitali ya Halmashauri ya Mji Kahama,kwa madai ya kukutwa akiuza kinyume cha taratibu dawa na vifaa tiba vya Serikali vyenye thamani ya Shilingi 106,000/-kwa mfanyabiashara wa duka la madawa.
Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi mkoa wa Shinyanga,Mika
Nyange,alimtaja Mtumishi huyo kuwa ni Egbart Kahugya,ambapo alikamatwa akiwa
katika mgahawa mmoja mjini Kahama akiwa katika harakati za kuuza kwa
mfanyabiashara mmoja wa maduka ya dawa.
Kamanda Nyange alisema mtuhumiwa huyo baada ya kuwekwa chini ya
ulinzi ulifanyika upekuzi katika gari yake iliyokuwa kanda ya Mgahawa huo na
kukutwa na mzigo huo wa madawa,na kwamba Polisi Mjini Kahama,bado inafanya
uchunguzi wa kina juu ya tukio hilo kwa kuwahoji watuhumiwa wote wawili,kabla
ya kuwafikisha Mahakamani kwa hatua zaidi za kisheria.
Kwa upande wake Mganga Mkuu katika Hospitali ya Halmahauri ya Mji
wa Kahama,Bruno Minja,alishtushwa na kittendo hicho cha Tabibu Kahugya kufanya
vitendo vya kibadhirifu ambapo alidai uongozi wa hospitali utachukua hatua
stahiki za kimaadili juu ya mtumishi huyo.
Dk.Minja alisema tayari wamechukua hatua za kisheria kwa kufungua
kesi kwa tabibu Kahugya,kwa kosa la kupatikana na dawa za serikali kinyume cha
sheria kwa kufungua jalada lenye namba KAH/IR/683/2016,baada ya kujiridhisha na
kuwaonya vikali watumishi wake wasiowaaminifu,kuondokana na tabia
ya wizi wa madawa na badala yake wafanye kazi kwa uadilifu.
Mganga Mkuu huyo alisema baada ya kukamatwa kwa tabibu huyo,kwa
kushirikiana na Polisi walifika Hospitalini hapo na mzigo huo na kubaini madawa
hayo na vifaa tiba yapo katika makundi matatu ambapo kundi la kwanza ni dawa za
serikali, la pili ni dawa halali, na la tatu ni dawa ambazo
hazijasajiliwa ambazo usajili wake ulifutwa na mamlaka ya chakula na dawa
“TFDA”.
Dr.Minja alifafanua kuwa katika mzigo wa dawa za Serikali
alizokamatwa nazo tabibu huyo ni aina ya Benzyl Penicillin zenye thamani ya TSh
22200/- na Hemocue HB Covettes zenye tahamani ya TShs 83800/-huku mzigo ungine
ukiwa ni ule wa madawa ambayo hupatiwa kwa msaada.Na ule ambao ulifutwa na TFDA
thamani yake ukiwa haijulikani.
Aidha alisema tukio hilo limedhihirisha kuwa kuna baadhi ya
watumishi katika hospitali hiyo si waadirifu na hufanya kazi kwa mazoea,na
kujinufaisha binafsi na kusahau maslahi ya Taifa, hali ambayo amedai
haikubaliki na kama wataendelea kufanya hivyo wataishia pabaya kutokana na
serikali ya sasa kutumia nguvu kubwa kuthibiti wizi wa dawa.