Monday, December 28, 2015

WAJAWAZITO NYANGH’WALE WAPATA AHUENI YA KUJIFUNGUA.

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO

ZUWENA Senkondo akimkabidhi Neema Mhoja vifaa vya Ukunga.

WANAWAKE wajawazito katika Kata ya Mwingilo,wilayani Nyangh’wale mkoani Geita,huenda wakapata ahueni ya kujifungua salama kwa kuondokana   kuhudumiwa na wakunga wa jadi,baada ya  Mgodi wa Bulyanhulu uliopo wilayani Kahama kutoa vifaa vya kujifungulia katika zahanati yao.
 
Akipokea vifaa hivyo, Mratibu wa huduma ya Baba,mama na mtoto katika Halmashauri ya Nyangh’wale,Neema Mhoja,alisema vifaa hivyo ambavyo ni seti nane,vyenye thamani ya Shilingi Milioni tatu vitawasaidia uzazi salama akina mama wajawazito katika eneo hilo na kuepusha vifo vinavyozuilika.
 


Awali Muuguzi katika zahanati hiyo ya Mwingilo,Consatine Matata,alisema vifaa hivyo vitaondoa tatizo la akina mama kujifungulia majumbani ama kukimbilia kwa wakunga wa jadi,kutokana na zahanati hiyo kutokuwa na vifaa vya kutosha kutumia wakati wa kujifungua.
 
“Akina mama walikuwa wakishindwa kufika   zahanati   kujifungua,nasi kuwa na wakati mgumu kuwapatia huduma  kutokana na kutumia kifaa kimoja,ililazimika kusubiriana baada ya kutumika  kukichemsha ndipo kutumika tena,hali hii iliwakatisha tama wengi wao kuja kujifungulia Zahanati,”alisema Matata.
 
Kabla ya hapo Meneja Mahusiano ya Jamii wa Mgodi wa Bulyanhulu unaomilikiwa na Kampuni ya Acacia,Elias Kasitila,alisema waliamua kutoa vifaa hivyo kwa lengo la kuimarisha ujirani mwema  baina ya Mgodi huo unaomilikiwa na Kampuni ya ACACIA,uliopo wilayani Kahama na kata hiyo iliyo wilayani Nyangh’wale.
 
Alisema mbali ya  kudumisha mahusiano ya ujirani mwema,pia wanazingatia kuwa wanawake wajawazito afya zao ni nguzo ya msingi wa maendeleo katika taifa,hivyo wanapaswa kulea mimba zao na kuwaandalia mazingira bora yatakayowafanya wajifungue salama.
 
Aidha Kasitila alisema walitoa vifaa hivyo baada ya kupokea maombi ya wananchi wa vijiji vya Iyenze na Mwasabuka katika kata hiyo ya Mwingilo,ambao walielezea athari zinazowapata wakina mama wajawazito wakati wa kujifungua. Vifaa vilivyokabidhiwa vina thamani ya Shilingi Milioni Tatu, vilitolewa katika zahanati ya  
 
Kwa upande wake Afisa Mahusiano ya Jamii wa Mgodi huo,Zuwena Senkondo,aliwaasa Wakunga katika Zahanati hiyo kuhakikisha vifaa hivyo wanavitumia vyema na kufikia matarajio ya Mgodi huo kutoa vifaa hivyo kwa lengo ya kuwasaidia  akina mama Wajawazito katika Kata hiyo kujifungua salama.

KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI