Monday, December 28, 2015

VIONGOZI WA SHULE KAHAMA WAREJESHA FEDHA WALIZOTAFUNA.

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO

            
WAZIRI wa Elimu,Sayansi,Teknolojia na Ufundi;Dkt.Joyce Ndalichako.
   
KASI ya kufichua wabadhirifu na Mafisadi inayotekelezwa na Rais wa Awamu ya Tano Tanzania,Dkt.John Magufuli,imeungwa mkono kwa vitendo na wazazi wilayani Kahama baada ya kufichua ufisadi katika Shule ya Msingi Kilima A,na kuwashinikiza wahusika warejeshe fedha zao.
 
Katika kikao cha wazazi katika shule hiyo,kilibaini Mwenyekiti wa kamati ya Shule, Simon Soka,pamoja na Mwalimu Mkuu wake, Lilian Lotasorwaki,walibainika na tuhuma za kutumia vibaya fedha za wazazi zaidi ya Shilingi Milioni tatu.
 
,kwakufanya ufisadi wa zaidi ya shilingi milioni tatu wameanza kurejesha fedha hizo .


Akiongea na Tanzania Daima,Diwani wa Kata ya Nyihogo, Shadrack Mgwabi,alisema wiki iliyopita wazazi walibaini matumizi mabaya ya fedha walizochanga kwa ajili ya maendeleo ya shule hiyo hivyo kuchukua maamuzi ya kuwazuia kuendelea  kufanya kazi katika shule hiyo huku wakiagiza fedha hizo kurejeshwa.
 
Mwenyekiti wa Shule hiyo,Soka,alisema maagizo ya wazazi hayo wameanza kuyatekeleza kwa kuanza kurejesha fedha hizo,huku akikanusha kuhusika na matumizi mabaya ya fedha hizo kwa madai alizitumia ikiwa ni moja ya utekelezaji wa majukumu yake.
 
Hata hivyo pamoja na Soka kukanusha tuhuma hizo,Mwalimu Mkuu wa Shule hiyo,Lotasorwaki,alimtwisha mzigo Soka akimtuhumu kumlazimisha ampe fedha hizo hali ambayo iliwafanya wazazi wawashutumu wote wawili kuhusika na matumizi mabaya ya fedha hizo.

Awali Kaimu Ofisa Mtendaji wa Kata ya Nyihogo,Simon Mabumba, alisema watuhumiwa hao katika mkutano wa wazazi wametuhumiwa kutumia fedha hizo kinyume na taratibu ambazo wazazi walichanga kwa ajili ya kununulia matofari .


Mabumba alisema katika mkutano huo wazazi hao  walimvua madaraka Mwenyekiti huyo wa shule ya msingi Kilima A huku  wakitaka hatua kali zichukuliwe dhidi ya wote hao wawili ambao wamehusika na upotevu wa fedha hizo.
 
Kufuatia hali hiyo wazazi hao walipitisha maazimio kwenye kikao hicho cha kuwachukulia hatua za kisheria viongozi hao wa shule hiyo ambao sasa kwa mujibu wa diwani Mgwabi juzi tayari walianza kurejesha kiasi cha shilingi milioni mbili na fedha zilizobaki wanaendelea kuzilipa.

KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI