KATIKA kuhakikisha
inadhibiti magonjwa ya milipuko inayotokana na kukthiri kwa uchafu,Serikali imeamua
kutangaza rasmi; kila Jumamosi ya mwisho
wa mwezi kuwa siku ya usafi Nchi
nzima.Kauli hiyo ilitolewa jana na Naibu Waziri wa Mazingira na Muungano,Luhaga Mpina, kwa niaba ya Waziri mwenye dhamana; January Makamba.
Naibu Waziri huyo alitoa
agizo kwa wakuu wa wilaya na wakuu wa mikoa kuhakikisha wanafanikisha jambo
hili na kuhakikisha mazingira yanakuwa safi kila siku.
Alisema suala hilo la usafi kuwa endelevu kwa kuwaagiza Wakurugenzi Watendaji katika Halmashauri za Manispaa,Miji na wilaya,kuhakikisha wanafanikisha zoezi hili kwa kuwaongoza wanaowaongoza kulifanya zoezi hilo kwa ufasaha.
Alisema suala hilo la usafi kuwa endelevu kwa kuwaagiza Wakurugenzi Watendaji katika Halmashauri za Manispaa,Miji na wilaya,kuhakikisha wanafanikisha zoezi hili kwa kuwaongoza wanaowaongoza kulifanya zoezi hilo kwa ufasaha.
Alisisitiza kuwa Serikali
itawawajibisha mara moja,watendaji watakaozembea na kushindwa kusimamia zoezi
hilo.
Aidha Waziri Mpina alisema
kila mwananchi itamlazimu kuwajibika siku hiyo,kwa kufanya usafi katika eneo
lake ili kuhakikisha mazingira yake yanaondokana na urafiki wa kukaribisha
magonjwa ya milipuko.
Zoezi rasmi linaanza
jumamosi ya mwisho January 2016.