Friday, December 25, 2015

HALMASHAURI MASUMBWE YAMCHAFUA MAGUFULI

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO

SIKU Rais Dkt.John Pombe Magufuli alipoongoza Watanzania kufanya Usafi.
HALMASHAURI ya wilaya ya Masumbwe imeshindwa kutekeleza ipasavyo zoezi la usafi lililofanyika nchi nzima 9 Desemba Mwaka huu,baada ya kutekeleza zoezi hilo kwa kukusanya uchafu na kushindwa kuuhifadhi ipasavyo,badala yake umeutelekeza Kijijini Shenda katika Kata ya Masumbwe wilayani Mbogwe mkoani Geita na kusababisha wanakijiji hicho kuingiwa hofu kuibuka magonjwa ya mlipuko wa magonjwa kupitia uchafu huo.
 
BAADHI ya Wakazi wa Kijiji cha Shenda wakishangaa Uchafu.
Kufuatia hali hiyo,ambayo imetafsiriwa  na baadhi ya Wanakijiji hao   kama ni kumchafua Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dkt.John Pombe Magufuli,aliyeagiza kumbukumbu za Uhuru wa Tanganyika kuzitumia kwa kufanya usafi nchi nzima,hivyo kuitaka ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mbogwe kuziondoa takataka zilizowekwa kijijini kwao.
 
 WANAKIJIJI cha Shenda wakistaajabu Uchafu.
Wakiongea na waandishi wa habari za mtandaoni   wanakijiji hao wamesema kuwa wanashangazwa na kitendo cha halmashauri ya wilaya kutuma takataka katika kijiji chao licha ya kwamba hakuna dampo la uchafu eneo hilo.
 
Wameongeza kuwa taka hizo ni hatari kwa afya zao kwani zimetupwa karibu na eneo la shule ya msingi,Makazi ya watu na vibanda vya mama ntilie hali inayozua hofu ya kuzuka kwa magonjwa ya mripuko,kutokana na taka hizo kuanza kuoza na kusambaa katika makazi ya watu kipindi hiki cha masika.
 
BAADHI ya Wanakijiji cha Shenda wakishangaa Uchafu.
Sambamba na hayo wameshangazwa na maamuzi ya ofisi ya Mkurugenzi kutupa taka hizo katika kijiji chao licha ya kuwa yapo maeneo mengi ya wazi ambayo yangeweza kutumika kutupa taka hizo ambazo kwa sasa zimekuwa kero katika kijiji chao hasa kwa kutoa harufu mbaya zinazoambatana na funza.
 
 
Kwa mujibu wa Kaimu Afisa Mtendaji wa kijiji cha Shenda, Joseph Jaseda, amesema sehemu zilizotupwa taka hizo ni makazi ya watu na kwamba walipouliza kuhusu hatua hiyo waliambiwa kuwa gari la kuzoa taka liliharibika hivyo kulazimika kutupa taka hizo katika maeneo hayo.
 
Kwa upande wake diwani wa kata ya Masumbwe, Shimo Kiyuyu amesema kuwa alifikisha malalamiko ya wananchi kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Mbogwe,akatoa gari ili uchafu uzolewe lakini juhudi hizo ziligonga mwamba kutokana na gari hiyo kwenda eneo la uchafu bila wazoaji wa taka hizo.
 
Kwa upande wake Afisa Afya wa halmashauri ya wilaya ya Mbogwe,Edward Razalo,amekiri uchafu huo kutupwa katika maeneo hayo na kuongeza kuwa baada ya wananchi kulalamika walienda kuweka dawa ya kuuwa wadudu katika taka hizo na kwamba hawajazihamisha kutokana na taka hizo kutokuwa na madhara kwa wananchi.

KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI