MMOJA wa Wachimbaji hao,Amosi Mhangwa{25} |
waliokolewa wakiwa hai huku hali zao zikiwa mbaya baada ya kuishi ardhini kwa siku 41.
Akiongea kwa tabu mmoja wa
wachimbaji hao,Chacha Wambura{54},ambaye pamoja na wenzake wamelazwa katika Hospitali
ya Halmashauri ya Mji wa Kahama,alisema baada ya kukatika kwa kifusi hicho
kiliziba njia ya kutokea,na kuwalazimu kujificha kwenye kona ya mashimo hayo.
Wambura alisema katika
machimbo hayo huchimba maeneo ya uwazi kwa ajili ya kuhifadhi vifaa vyao vya kazi
ndiko walikojificha na kujinusuru na uhai wao kwa kutopandwa na vifusi na
waliishi kwa kula chura,wadudu kama mende,mijusi na ambao waliamini hawana sumu ya kuwdhuru
pamoja na mizizi,magome ya miti na kunywa maji.
.
Wambura alisema walikikutwa na maafa hayo yeye
na wenziwe watano,baada ya kuwaokoa wachimbaji wenzaao na walimudu kwenda
katika moja ya vyumba hivyo ndani ya mashimo hayo na kuanza kutafuta njia ya
kutokea wakitumia mwanga wa tochi na simu zao za mkononi kabla hazijaishiwa
moto.
Hata hivyo awali wakati
tukio hilo likitokea Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Mgodi huo uliotitia
wa Shigomico,Hamza Tandiko,alidai ufukuaji wa eneo hilo ulihitaji gharama kubwa
kutokana na kuwa wamefukiwa umbali wa zaidi ya mita 100.
Tandiko alisema kutokana
na gharama kuwa kubwa iliwalazimu kuanza mkakati mpya kwa kushirikiana na
serikali kuwafukua watu hao ambao tayari familia zao walizitangazia msiba
kutokana na kuhisi waliishapoteza uhai wao.
Hata hivyo wakati Serikali
ikiwa na mkakati huo wa kuwatoa kwa kufukua eneo hilo kule chini waathirika hao
walikuwa wakifanya juhudi binafsi za kujiokoa kwa kupenyeza katika maeneo
mengine yaliyoingiliana kule chini ya ardhi.
CHACHA Wambura akiwa amelazwa kwa matibabu zaidi. |
Wambura alisema baada ya
kuona hali hiyo waliendelea kutafuta njia ya kutokea lakini baada ya siku saba
matumaini yalianza kuisha kutokana na wao kuanza kuchoka na pia njaa iliwakaba
kiasi cha kuishiwa nguvu na kubaki kutegemea kudra za Mwenyezi Mungu.
Pia alisema baada ya hapo
wakiwa huko chini,waliona Mwanga lakini ukiwa umezibwa na jiwe kubwa hali ambayo
ilizidi kuwakatisha tamaa ya kutoka,ingawa sasa kuna eneo waliona chemic hemi ya
maji yakitiririka,nakutumia kofia ngumu kukinga na kunywana na kipindi chote
walishirikiana kuokoa uhai wao.
Alizidi kufafanua kuwa katika
mashimo kuna miti inayofungwa kama nguzo ya kushikilia ukuta wa Shimo,ambayo walikuwa wakiyabandua maganda yake na kuchimba
kiini chake cha ndani na kula,huku wakati mwingine wakikamata wadudu kama vile Mende
na kula.
Kwa masikitiko alimtaja mwenzao mmoja,Mussa Supana ambaye aligoma kula aina hiyo ya chakula hali
iiliyosababisha siku kumi na tano kabla hawajaokolewa apoteze maisha yake,na
wakati huo hali ya uhai kwaoilikuwa ngumu kutokana na vifaa walivyotumia kupata
mwanga kama simu betri zake kuisha chaji.
Aidha alisema kuna siku walisikia
sauti za wachimbaji wengine wakiendelea na uchimbaji kwenye mashimo mengine
kule chini lakini walipopiga kelele ya kuomba msaada watu hao waliondoka moja
kwa moja hadi alipotokea huyo mmoja ambaye walijibizana nae na kuwaaahidi
kuwasaidia.
Baada ya muda ndipo
waliposikia milio ya sauti ya wachimbaji wakitoboa njia mpaka kuwafikia
walipokuwa na ikawa sasa wameokolewa ingawa mmoja wao tayari alikuwa amekwisha
fariki lakini waliwaeleza hali hiyo ya mwenzao huyo,kufariki.
Mganga
Mfawidhi wa Hospitali hiyo Joseph Ngowi,alithibitisha kuwapokea watu hao, Chacha
Wambura,Amosi Mhangwa{25},Joseph Bulule Rhobi{44},Msafiri Gelard na Onyiwa Moris
{55}na kudai wanaendelea na jitihada za kuokoa uhai wao.
Ngowi alisema hali zao
zinaendelea vizuri ingawa kwa sasa hawawezi kula chakula kutokana na utumbo wao
kusinyaa,huku nuru za macho yao yakiwa hafifu kutokan na kuishi muda mrefu
gizani .
Ngowi alisema kwa kawaida
mtu akiishi bila kula chochote na akiwa na afya nzuri anaweza kufa ndani ya
siku 14,lakini hawa wamedumu kwa siku 41 kutokana na kula chakula kisicho
halisi huku hali ya lishe mwili ilikwisha na walikuwa wakiishi kwa lishe ya protini
ya misuli.
Pia Ngowi alisema watu hao
hali zao zakawaida zinaweza zikarejea baada ya siku saba kutokana na kuwa chini
ya uangalizi wa wataalamu mbalimbali wakiwemo wa lishe, mazoezi ya viungo na
saikolojia.
Kwa upande wake Kaimu
Kamishina wa Madini Tanzania,Ally Samaje,alisema tukio hilo limewakuta wakiwa
safarini kwenda kwenye machimbo hayo kwa lengo la kutaka kulifukua eneo hilo,na
kuwaomba wachimbaji wadogowadogo wazingatie taratibu za usalama pindi
wanapokuwa katika shughuli za uchimbaji kwa ajili ya kupata dhahabu na kuuza
kwa lengo la kupata fedha peke yake.