Sunday, November 29, 2015

UCHIMBAJI SALAMA KUIMARISHWA MIGODI MIDOGO

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO



ADHA za wachimbaji wadogo kufunikwa na vifusi katika migodi wanapokuwa katika shughuli za kutafuta mali,huenda ikapungua
kutokana na Chama cha wachimbaji wadogo mkoani Shinyanga “SHIREMA”,kuanza kutoa Elimu ya uchimbaji salama kwenye migodi yake.

Mkaguzi mkuu kutoka chama hicho,Amos Mbaga,amebainisha hayo jana alipoongea na CGFM,kwa kueleza kuwa timu ya Wataalamu wa Uchimbaji salama kutoka SHIREMA,imeanza kuzunguka migodi yote kutoa Elimu hiyo.

Amesema wameona umuhimu wa kutoa Elimu hiyo,baada ya mapema mwezi uliopita,Machimbo katika mgodi wa Nyangalata wilayani Kahama kutitia na kuwafunika wachimbaji zaidi ya 11 ambao wengine waliokolewa na kubaki watano ambao baadaye waliokolewa baada ya kuishi ardhini kwa siku 41

Hata hivyo Elimu hiyo imekuja baada ya mkaguzi mkuu kutoka wizara ya nishati na Madini Ally Samaje kuagiza migodi yote imarishwe ili wachimbaji hao wachimbe kwa usalama zaidi

Samaje ambaye alikuwa mjini Kahama akimuwakilisha Kamishina wa Madini Tanzania amewataka viongozi wote wa chama hicho pamoja na wa migodini kutoa Elimu ya usalama wakati wa uchimbaji madini kwenye machimbo hayo


KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI