Friday, November 27, 2015

KAFULILA USO KWA USO NA JAJI ALIYEHUKUMU TEGETA ESCROW

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO




KESI ya kupinga matokeo ya Ubunge katika uchaguzi Jimbo la Kigoma Kusini iliyofunguliwa na aliyekuwa Mgombea Ubunge wa Chama cha NCCR-Mageuzi,aliyeungwa mkono na vyama vya Umoja wa Katiba ya Wananchi "UKAWA",David Kafulila,imeaanza kusikilizwa jana na Jaji John Utamwa katika Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Tabora.

Kafulila aliyekuwa Mbunge kinara katika kuibua ufisadi wa sakata la uchotwaji wa zaidi ya Sh. bilioni 306 katika akaunti ya Tegeta Escrow iliyokuwa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), anakutana ‘uso kwa uso’ na Jaji Utamwa, ambaye ndio alitoa hukumu tata iliyosababisha kuibuka kwa kashfa ya ufisadi wa fedha hizo.

Jaji Utamwa aliitoa hukumu hiyo, Septemba 8, 2013 kwa kumwamuru Kabidhi Wasihi, kukabidhi mtambo wa Kampuni ya kufua umeme wa dharura ya Independent Power Tanzania Limited (IPTL) kwa mmiliki wake mpya ambaye ni kampuni ya Pan Africa Power Solutions Tanzania Limited (PAP) baada ya kukubaliana na maombi ya aliyekuwa mbia wa IPTL, kampuni ya Engineering and Marketing Limited (VIP) iliyoondoa kesi yake kwa lengo la kuifilisi IPTL.

Hukumu hiyo ndio ilikuwa chanzo cha Kafulila kuibua kashfa hiyo bungeni kwa kuwahusisha vigogo mbalimbali wa serikali na ufisadi huo.

KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI