Friday, December 5, 2014

WENJE AMSHANGAA KINANA KULALAMA JUU YA SERIKALI.

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO



MBUNGE wa Jimbo la Nyamagana mkoani Mwanza,Ezekiel Wenje amemshangaa Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi Taifa, Abdurahmani Kinana kila mara kulalamika juu ya Utendaji mbovu wa Serikali inayotawaliwa
na Chama chake.

Wenje ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama cha Demokrasi na Maendeleo “CHADEMA”Taifa,alitoa kauli hiyo kwenye mkutano wa uzinduzi wa Kampeni za Uchaguzi wa Serikali za Mitaa katika Jimbo la Musoma Mjini zilizofanyika katika viwanja vya Shule ya Sekondari Mara.

Mbunge huyo wa Nyamagana alisema Kinana na chama chake hawawajibiki juu ya Serikali zaidi ya kubakia kulalamika kuwa ndani ya Serikali kuna watendaji wabadhirifu wakiwemo Mawaziri mizigo wanaoipeleka nchi mrama huku akiwa na nguvu ya kumshauri Rais,kwakuwa ni Mtendaji Mkuu wa Chama kinachotawala nchi.

“Kinana yupo karibu na Mwenyekiti wake wa CCM Taifa ambaye ni Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania,Kikwete ni vipi kashindwa kumshauri kuwang’oa na kuisafisha Serikali na kashfa mbalimbali sambamba na kuboresha utendaji utakuwa tija kwa wananchi,lakini amebakia kulalama hii ni dalili tosha wenzetu hawa wamechoka na hawana jipya.”Alisema Wenje.


Aidha aliwaomba Wakulima ambao hapa nchini hawana hadhi katika kilimo chao kutokana na sera mbovu za CCM kujitambua na kuongoza mabadiriko ya kuindoa madarakani CCM kuanzia ngazi ya Serikali ya Mitaa hadi Uchaguzi Mkuu ujao na kukichagua CHADEMA ambacho kimepanga kuwakomboa kiuchumi Wakulima,ili  watoe mchango wa maendeleo ya nchi.


“CCM inatia aibu Serikali yake inaomba misaada hadi katika nchi ambazo Mawaziri wake wanazidiwa wingi na ufahari wa magari na Mawaziri wetu,wameshindwaje kuboresha uchumi wetu na kumpatia kila Mtanzania maisha bora kama si ufisadi tu wanaoufanya,”Alisema Wenje.




Kwa upande wake Mbunge wa jimbo la Musoma Mjini,Vicent Nyerere alisema uongozi wa CCM umetawaliwa na ufisadi,na upinzani una dhamira ya dhati ya kutetea maslahi ya Taifa kama ambavyo UKAWA walivyomudu kufichua juu ya Akaunti ya Tegeta Escrow.

“Tutaendelea kuwaumbua ufisadi wao,na Januari mwaka 2015 tunakuja na sakata la sukari ambalo ni zaidi ya Escrow,”Alisema Mbunge Nyerere.

Mbunge Nyerere alisema hayuko tayari kuona wananchi wa Jimbo lake wakikamuliwa kwa kutozwa michango mbalimbali ikiwemo ya maabara  ilhali waliishatozwa kodi katika bidhaa mbalimbali zikiwemo leseni za udereva,biashara,soda,sukari na nyinginezo.

Awali akifungua mkutano huo,Diwani wa Kata ya Nyamatare,Alex Kisirula ambaye pia ni Meya wa Manispaa ya Musoma kwa tiketi ya CHADEMA alisema jitihada zimefanyika kupitia kwa wahisani kujenga uzio na kufanya ukarabati katika Shule ya Msingi Mwiseng,ambayo ina wanafunzi wenye ulemavu mbalimbali .

Kisirula alisema wahisani wameishatoa kiasi cha Shilingi  kwa ajili ya kuweka umeme zaidi ya shule tisa za sekondari jimboni humo pamoja na uzio wa Shule hiyo ya Msingi Mwiseng ambapo zimetengwa zaidi ya Shilingi Milioni 240,huku wakitarajia kukamilisha ujenzi wa vyumba vya maabara kwa gharama ya Shilingi Milioni 409.

CHADEMA Jimbo la Musoma Mjini kimesimamisha jumla ya wagombea  nafasi ya Uenyeviti wa Mitaa 71 wanaotarajiwa kupigiwa kupigiwa kura Desemaba 14 mwaka huu,huku mgombea wake mmoja miongoni mwao akiwekewa pingamizi Mahakamani na CCM kwa tuhuma za kukikashfu chama hicho mara alipokihama mapema mwezi Oktoba mwaka huu.

Chanzo cha Habari ni Kepha Masatu – Musoma

KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI