Tuesday, December 2, 2014

MWANASOKA WA ALGERIA ATWAA TUZO YA BBC

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO

Kiungo wa Kimataifa wa Algeria, Yacine Brahimi(24) amekuwa raia wa kwanza wa Algeria kutwaa Tuzo ya Mwanasoka Bora wa Afrika kwa 2014 kama
ilivyoendeshwa na Shirika la Utangazaji la Uingereza (BBC).

Brahimi  anayechezea Porto ya Ureno ametwaa tuzo hiyo baada ya kupigiwa kura na washabiki wa soka,waliovunja rekodi ya upigaji kura kutoka nchi 207 zilizosajiliwa na Shirikisho la Soka la Kimataifa (Fifa).

Mwanasoka huyo ametwaa tuzo hiyo baada ya kuwashinda kipa wa Timu ya Taifa ya Nigeria, Vincent Enyeama; mchezaji wa Gabon, Pierre-Emerick Aubameyang, Gervinho na Yaya Toure wote wawili wa Ivory Coast. Toure aliitwaa tuzo hiyo mwaka jana.

Baada ya kutwaa tuzo hiyo Brahimi alisema ni heshima kubwa kwake kupata tuzo hiyo ambayo ameamua kuitoa kwa ajili ya nchi yake na watu wote waliomchagua, akisema pia kwamba ni kombe kwa watu wote wa Afrika.

Alisema kombe hilo litampa nguvu na ari ya kufanya kazi kwa bidii zaidi, kuwa mzuri ndani na nje ya dimba ili aweze pamoja na timu anazotumikia, kupata mafanikio makubwa. Msimu uliopita aling’ara sana kwa klabu na nchi yake.

KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI