Tuesday, December 2, 2014

HUHESO KUFAIDISHA WATU ELFU 12 MRADI WA PESA KWA WOTE

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO

 MWENYEKITI wa Halmashauri ya Mji wa Kahama;Machibya Kidulamabambasi.

 SHIRIKA la HUHESO FOUNDATION  la mjini Kahama mkoani Shinyanga linatarajia kuwafikia watu 12,178 kwa lengo la kuwawezesha elimu elimu juu ya kuanzisha vikundi vya kujiwekea kisha kukopeshana fedha,ili kujiletea maendeleo katika familia zao na Taifa kwa ujumla.


WASHIRIKI wa utambulisho wa Mradi wa Pesa kwa wote.

Hayo yalielezwa na Mkurugenzi wa Shirika hilo Juma Mwesigwa wakati akitambulisha Mradi wa Pesa kwa Wote (PKW) kwa wakuu wa idara mbalimbali,maafisa watendaji wa kata pamoja na maafisa maendeleo ya jamii wa  Halmashauri zote  tatu za  wilaya ya Kahama,ambapo mradi huo utatekelezwa kwa kipindi cha miaka minne.

MENEJA MRADI na Mkurugenzi wa Shirika la HUHESO FOUNDATION;Juma Mwesigwa akifafanua jambo.      


Mwesigwa alisema mradi huo umefadhiliwa na Cooperative for Assistannce and Relief Everywhere,inc,(CARE)in Tanzania  ambao utatekelezwa katika mikoa saba hapa Tanzania ikiwemo Morogoro,Pemba na Unguja(Zanzibar)na mikoa ya kanda ya ziwa Mwanza,Tabora na Shinyanga.


Alisema kwa upande wa Shinyanga ni utatekelezwa katika wilaya za Shinyanga vijijini, Kishapu na Kahama.Ambapo  kwa upande wa wilaya ya Kahama mradi huo utahusisha  Halmashauri zote tatu Halmashauri ya mji wa Kahama,Msalala na Ushetu na Shirika lake litahusika na kuutekeleza.

“Lengo ni kuwafikia watu 12,178 kwa  miaka minne kwa Kahama, na tumepewa majukumu ya kutekeleza mradi huo kwa kufadhiliwa  m.45,206,500 kwa  mwaka wa kwanza ,na mkataba wake unanzia Octoba 01,2014 hadi Juni 30,2015.”Alisema Mwesigwa.
MWENYEKITI wa Bodi ya Wakurugenzi wa Shirika la HUHESO FOUNDATION;Shija Felician.

Hata hivyo mratibu wa mradi huo katika shirika hili,Fatuma Shabani naye alisema malengo ya mradi wa pesa kwa wote ni kuwajengea uwezo wanakikundi ili waweze kujiwekea akiba kwa malengo ya kuongeza uhakika wa kipato kupitia kujiwekea akiba zao, mfuko wa jamii na kutoa mikopo kwa wanachama kwa ajili ya maendeleo.



Alisema mradi huo utawafikia wanawake kwa asilimia70 na wanaume asilimia 30 ya idadi yote ya wanachama,kutoka katika jumla ya vikundi 487 kwa miaka yote minne katika Halmashauri zote tatu za Kahama kutoka kwenye kata 15 .
MMOJA wa washiriki katika Utambulisho huo,Afisa Maendeleo katika Halmashauri ya Wilaya ya Msalala;Aliadina Peter akitoa machango wake juu ya kuboresha Mradi wa Pesa Kwa Wote.
Aliongeza mradi huo utasaidia wananchi wa vijijini ambao kwa kiwango kikubwa kuna na ukosefu wa huduma za kifedha,sambamba na ugumu wa masharti ya mikopo kutoka Mashirika ya kifedha ambayo pia huwapa wakati mgumu wa kurejesha mikopo kutokana na ukubwa wa riba jambo linalotoa wakati  mgumu wa kufuata na kukamatiwa mali kwa anayeshindwa kulipa.


“Tunautambulisha rasmi mradi wa pesa kwa wote na hilo ni jina tu siyo kwamba tunasambaza pesa,Shirika hili litawajengea uwezo wanakikundi ili waweze kukopeshana wenyewe,ambapo tutawahamasisisha kwa kufanya mikutano ya hadhara kupitia Watendaji wa kata na vijiji hadi mitaa,ili wamudu kuunda vikundi vya kukopeshana wenyewe kwa masharti nafuu,”Alisema bi Fatuma.

 

Kwa upande wake mwenyekiti wa halmashauri mji wa Kahama,Machibya Kidulamabambasi akimwakilisha mkuu wa wilaya hiyo,Benson Mpesya aliwataka shirika hilo kufanya kile walichokusudia na mradi huo usiishie mikononi mwa watu wachache kwani fedha nyingi zinazotolewa na wafadhili huwa haziwapati walengwa.


“Kwaniaba ya Serikali niwaombe mwendelee kushilikiana na idara za Halmashauri ya mji wa Kahama pamoja na kuwatumia maafisa maendeleo kuwahamasisha  wananchi kujiunga katika vikundi kuhusu mradi huo wa pesa kwa wote,”
DIWANI wa Viti Maalumu kwa tiketi ya CCM,Josephine Baranoga naye akitoa mchango wake.



Aliongeza;“ Kusudi mfadhili aendelee kusaidia wananchi lazima mjitume,msiwe kama mashirika mengine ambayo yamekuwa yakijinufaisha kupitia miradi mbalimbali inayotolewa na wafadhili, sisi kama halmashauri hatutaki kusikia ubabaishaji huo unatokea, nawashauri watu wajiunge makundi ili wapate mafunzo hayo iwe njia rahisi ya kukopeshana.”

KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI