MKUU wa Mkoa wa Kilimanjaro,Leonidas Gama. |
MAGARI tisa na nyumba 16 zimeteketezwa moto katika mgogoro ulioibuka kijiji cha Miti Mirefu ,
wilaya ya Siha mkoani Kilimanjaro
baina ya Wafugaji na Mwekezaji wa shamba la Ndarakwai chanzo kikiwa ni kugombea malisho.
baina ya Wafugaji na Mwekezaji wa shamba la Ndarakwai chanzo kikiwa ni kugombea malisho.
Ilibainika kuwa chanzo cha
uharibifu huo ni kugombea malisho baina
ya jamii ya kifugaji ya Kimasai na Mwekezaji katika shamba hilo kiasi cha kusababisha ugomvi hata kuzua hali ya wasiwasi
katika eneo hilo.
Vurugu hizo zilizuka hivi karibuni kati ya wafugaji jamii ya wamasai na Mwekezaji katika shamba la Ndarakwai, kijiji cha Miti Mirefu, wilaya ya Siha, mkoani Kilimanjaro na kusababisha uharibifu mkubwa wa mali huku mlinzi mmoja wa mwekezaji huyo akijeruhiwa vibaya kwa risasi.
MIONGONI mwa gari la Mwekezaji lililoteketea kwa moto |
Kwa mujibu wa Mashuhuda wa
tukio hilo walisema vurugu hizo zilizuka baada ya mifugo zaidi ya 300 ya
wananchi wanaokaa jirani na shamba la Ndarakwai Ranchi, linalomilikiwa na
Mwekezaji aliyefahamika kwa jina la Peter Jones, kukamatwa na walinzi wa shamba
hilo.
Afisa Mtendaji wa kijiji hicho, Israel Kileo alisema tukio hilo lilitokea majira ya saa 7:00 mchana, baada ya wafugaji kudaiwa kuingiza mifugo katika mashamba ya mwekezaji baada ya kukosa eneo la malisho maeneo ya vijijini.
Kileo alisema vurugu hizo zilihusisha wananchi kutoka wilaya za Longido na Siha ambapo wote kwa pamoja wanatafuta eneo la malisho huku baadhi wakidaiwa kutomtaka mwekezaji huyo ambaye anafanya utalii wa picha, kambi za watalii na kufuga wanyama kama Tembo,Twiga,Pofu na Nyani.
ASKARI wa kutuliza ghasia wakiwa eneo la tukio |
Naye mwekezaji huyo Peter Jones alielezea kusikitishwa na tukio hilo na kudai hajua sababu za msingi wala hasara iliyopatikana kwani aliondoka eneo la tukio huku akilazimika kusitisha safari za wageni zaidi ya 10 waliotakiwa kwenda kwa ajili ya utalii mwezi huu.
MWEKEZAJI wa eneo la Ndarakwai,Peter Jones |
Simeli aliongeza kusema hasira ya wafugaji ziliongezeka baada ya askari kuwapiga risasi vijana hao na kuwatelekeza porini hadi hapo walipoamua kumchukua na kumpeleka hospitali ya Kibong’oto na baadaye kuhamishiwa hospitali ya KCMC kwa ajili ya matibabu zaidi.
Akizungumzia tukio hilo, Mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa na mkuu wa mkoa huo, Leonidas Gama alisema serikali imesikitishwa na kitendo kilichofanywa na wafugaji hao na ameliagiza jeshi a polisi kuchukua hatua za kisheria dhidi ya wahusika.
Gama alisema katika tukio hilo wafugaji hao walichoma nyumba 16 za mwekezaji huyo ikiwamo kambi za watalii, magari 9 na kuvamia mashamba nane ambayo wameingiza mifugo kwa ajili ya malisho.
Alifafanua kuwa Mwekezaji huyo alikuwa akimiliki
ranchi yenye wanyama aina tofauti zaidi ya 65 ambao walikuwa wakiingia na
kutoka eneo hilo na kusaidia kuliingizia pato la kigeni taifa sambamba na kutoa ajira ya watu 76 ambazo atalazimika
kuzisitisha kutokana na kusimama kwa shughuli zake.
Aidha kamati za ulinzi na usalama za wilaya ya Siha na Longido zitakaa meza moja ili kujadili na kufikia mwafaka wa mgogoro huo Novemba 19, mwaka huu.