Thursday, July 24, 2014

KAHAMA YADHIBITI MASOKO YASIYO RASMI

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO

MKUU wa wilaya ya Kahama;Benson Mpesya akisisitiza jambo.
WAFANYABIASHARA  ndogo wanaofanya shughuli zao hizo katika masoko yasiyo rasmi katika Halmashauri ya mji wa Kahama wametakiwa kuondoka mara moja na kuhamia
eneo rasmi kabla hawajaondolewa kwa nguvu katika Oporesheni inayoendelea Mjini Kahama.

Agizo hilo lilitolewa juzi na Mkuu wa wilaya ya Kahama Benson Mpesya wakati alipotembelea na kuongea na wafanyabiashara wa soko jipya la Mayila lililopo Kata ya Nyihogo,na kuwaeleza changamoto zilizopo katika eneo hilo kuwa zitashughulikiwa kwa wakati.

Mkuu huyo wa wilaya alisema anatambua changamoto zilizopo sokoni hapo zikiwemo za miundo mbinu za barabara za kufika hapo hata hivyo alibainisha si kigezo cha kuanzisha masoko yasiyo rasmi kwakuwa serikali haina utaratibu wa kila mtu kuanzisha soko lake kadri anavyotaka mwenyewe.

Mpesya alisema Halmashauri ya Mji tayari ina maeneo ambayo imejenga masoko ambayo kuwepo kwake kwa Wafanyabiashara hao kuwataka kuhamia katika maeneo hayo rasmi hatua itakayosaidia utunzaji mzuri wa usafi wa mji na upatikanaji wa ushuru unaosaidia maendeleo ya Mji.
Hivyo aliwaomba wananchi kumpatia orodha ya masoko yasiyo rasmi ikiwemo soko la kwa Mlapa lililopo kati ya Kata za Mhungura na Nyihogo ambayo licha ya wafanyabiashara wake kuondolewa wameanza kurudi na kuhadharisha kuwa wanaoendelea kukiuka taratibu pindi watakapokamatwa katika maeneo hayo wakifanya biashara watachukuliwa hatua kali za kisheria.

Kabla ya hapo Wafanyabiashara hao walimueleza Mkuu huyo wa wilaya kuwa wanashindwa kulipa ushuru katika Halmashauri ya Mji kutokana na biashara zao kuathiriwa na uanzishwaji wa masoko holela mitaani hali ambayo Mpesya amesema watu hao watakumbwa na oporesheni hiyo inayoshirikisha pia Jeshi la Polisi.

Kwa upande wake Diwani wa Kata ya Nyihogo Amosi Sipemba alisema wafanyabiashara hao wamewekeza zaidi ya Shilingi Bilioni Tatu katika soko hilo la Mayila ili serikali iweze kunufaika ni budi masoko ya mitaani yaondolewe hali ambayo Mkuu huyo wa wilaya amesema wataondolewa na kutakiwa kuhamia soko la Mayila.   

Akizungumzia soko la Wakulima Mkuu huyo wa wilaya alisema Wafanyabiashara katika eneo hilo lazima waondoke baada ya kukamilika kwa soko la Majengo kwakuwa eneo hilo Serikali hainufaiki na chochote wakati ikitumia gharama kubwa kusomba mrundikano mkubwa wa taka unaozalishwa toka ndani ya soko hilo.
           

KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI