Sunday, September 8, 2013

VIJANA WAASWA KUTOKIMBILIA NDOA PASIPO KUFAHAMU CHANGAMOTO ZAKE.

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO



Add caption

Add caption

Add caption

Add caption


Add caption

Add caption


 



VIJANA WAASWA KUTOKIMBILIA NDOA PASIPO KUFAHAMU CHANGAMOTO ZAKE.


IMEELEZWA kuwa kuvunjika kwa ndoa nyingi katika zama hizi zinavunjika na kusababisha kuwepo kwa wimbi la watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi kutokana na Vijana wengi kuingia katika maisha ya unyumba pasipo kujua changamoto zake.

Hayo yalielezwa na Mchungaji Jacob Ochola wa Kanisa la African Inland Church la Majengo wilayani Kahama,katika Jubilei ya miaka hamsini ya ndoa ya Mzee Mathias Mulela[77]na mkewe Esther Gombanila [69]wakazi wa Kata ya Majengo katika wilaya ya Kahama mkoani Shinyanga.

Mchungaji Ochola alisema ongezeko la watoto la mitaani linachangiwa na wana ndoa kutengana,kitendo kinachosababisha ukosefu wa umakini wa malezi ya watoto kutoka pande mbili za wazazi hivyo kuwalazimu watoto kuingia mitaani na kuanza maisha yasiyo na tija  na hatari kwa Taifa letu la baadaye.

Alisema kiini cha tatizo hilo ni kutokana na vijana wengi kujitumbukiza katika maisha ya ndoa wakiwa katika umri ndoa lakini wakijikuta wakifuata mkumbo wa kufunga pingu za maisha pasipo kuzifahamu na kujiandaa kukabiliana na changamoto za ndoa.

Hivyo aliwaasa vijana kutokimbilia maisha ya ndoa pasipo kufahamu changamoto zake ili kuepuka kutoheshimiana ambacho kimekuwa chanzo cha kuvunjika kwa ndoa nyingi na kulinusuru Taifa kuwa na kizazi cha watoto wa mitaani ambao mazingira ya maisha yao ni hatari kwa maendeleo ya Nchi.

Aidha aliwapongeza bwana na bibi Mulela kwa kufaulu kuvuka vikwazo vingi vya kimaisha ambavyo vingeweza kusambaratisha ndoa yao,na kusisitiza hiyo inatokana na wanandoa hao kuamua kufunga pingu za maisha huku wakiwa wanatambua changamoto za ndoa na kukubaliana nazo.





KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI