Wednesday, March 7, 2018

KAHAMA WATAKIWA KUTEKELEZA MAAMUZI YA LUKUVI

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO

Maamuzi na maelekezo ya Waziri wa wa Ardhi,Nyumba na Makazi,Wiliam Lukuvi,aliyoyatoa kwa Halmshauri ya Mji wa Kahama,imeshauriwa
yatekelezwe kwa haki.

Katika ziara aliyofanya hivi karibuni wilayani Kahama,kwa lengo la kutatua migogoro ya ardhi iliyokuwa imekithiri mjini Kahama na kusababisha kuwepo kwa kero ya muda mrefu kwa wananchi,Waziri Lukuvi alitoa maelekezo kadhaa kwa viongozi wa Halmashauri ya Mji na Serikali ya wilaya,.

Baadhi ya wananchi wakiongea kwa nyakati tofauti na maeneo mbalimbali ya mji wa Kahama, walipongeza utaratibu wa Waziri Lukuvi,kushughulikia migogoro ya ardhi kwa uwazi na kuomba serikali ya wilaya kutekeleza kwa haraka maagizo yake.

Mkazi wa Kata ya Malunga,Masumbuko Henry,alisema anampongeza Waziri Lukuvi kufika kushughulikia migogoro ya kipindi kirefu iliyokuwa kero,huku mingi ikiwa imesababishwa na watendaji katika Idara ya ardhi.

Aidha mkazi wa Mtaa wa Majengo,Nusura Maganga,alisema kuhusu eneo la soko la wakulima ambalo kwa kipindi kirefu limekuwa katika utata juu ya haki ya umiliki,ni vyema likapangiwa matumizi haraka ilisaidie kuipa mapato Halmashauri ya Mji wa Kahama.

Maganga aliiomba halmashauri ya mji wa Kahama inapaswa kuwaita na kuketi na wajasariamali ambao tayari waliishawekeza kwa kujenga vibanda vya biashara katika eneo hilo lililokuwa na utata wa umiliki uliosababisha kuikosesha mapato halmashauri.

Nae Salome Hussein mkazi wa Kata ya Nyasubi,aliomba halmashauri ya Mji kutumia fursa hiyo kuwaweka hapo wamachinga ambao wamekuwa wakizagaa mitaani kwa kufanya biashara katika maeneo yasiyokuwa rasmi.

Mmoja wa Mmachinga,John Samweli,alipendekeza eneo hilo lililokuwa la soko ni vyema likatumika kwa bidhaa za nguo za mitumba,vyombo na biashara ndogondogo nyingine kama ilivyo kwa wafanyabiashara waliopo Makoroboi Jijini Mwanza.

“ Nampongeza Lukuvi kuliresha eneo hilo serikalini ambalo baadhi ya wajanja wachache walikuwa wamejimilikisha na kujinufaisha na kusababisha kuikosesha mapato Serikali kupitia zaidi ya vibanda 100 vilivyojengwa kwa zaidi ya miaka 15 iliyopita,”alisema Samweli.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Kahama,Anderson Msumba alisema atahakikisha anasimamia haki baada ya eneo hilo kurejeshwa chini ya Halmashauri yake ili liweze kusaidia kuongeza vyanzo vya mapato  ya Serikali.

Msumba alisema kwa upande wa Wajasiriamali waliowekeza kwa kujenga vibanda vya biashara alisema atakaa nao na kuhakikisha anatenda  haki ili Halmashauri na serikali zipate mapato ambayo yatasaidia katika suala la maendeleo.



KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI