M
|
atukio ya mauaji ya dhidi ya
Vikongwe,watu wenye ualibino vinavyosadikiwa
kusababishwa na imani za
kishirikina,kutokomezwa pindi jamii itakapowekeza katika suala zima la elimu.
Mbali na matukio hayo,jamii ikielimika
itakuwa nyenzo muhimu ya kutokomeza vitendo vya kinyama vilivyokithiri vya
kutupa watoto wachanga mara wanapozaliwa.
Mkurugenzi wa Taasisi ya Elimu ya
Rocken Hill Academy,inayomiliki shule za Msingi na Sekondari wilayani
Kahama,Alexander Kazimil,amebainisha hayo katika mahafari ya 13 kwa shule za
msingi zilizo katika taasisi yake.
Ameisitiza katika dunia ya
Utandawazi,elimu ni nyenzo muhimu katika kustawisha familia na taifa,hivyo ni
vyema jamii ikatumia nguvu nyingi katika kuhakikisha rasilimali pekee
wanayowekeza kwa ajili ya vijana wao,inakuwa elimu.
Kazimil alisema jamii nyingi nchini bado
imeendelea na matukio ya mauaji
yatokanayo na ushirikina kwa vikongwe na albino huku vichanga vikitelekezwa kwa
kutupwa baada ya kuzaliwa kutokana na kukabiliwa na ombwe la kutoelimika.
“…naamini kupitia elimu,jamii
itaimarika kiuchumi na kuondokana na vitendo hivyo viovu,hivyo nasisitiza sana
wazazi wekezeni kwa watoto wenu elimu,kwani ndio silaha ya kupinga maovu,”anasema
Kazimil.
Anaendela kusisitiza katika kipindi
hiki cha upepo mkali wa Utandawazi,taifa litafikia malengo yake ya kuwa na
viwanda huku jamii yake ikiwa na uchumi wa kati pindi uwekezaji katika elimu
ukipewa kipaumbele,hasa kwakuwa Serikali imetoa fursa pana ya utoaji elimu bure
kuanzia chekechea hadi darasa la kumi na mbili.
Aidha alisema ili kujenga taifa lenye
watumishi wazalendo,ni budi wazazi na taasisi za elimu zikashirikiana katika
kuhakikisha linawalea vijana katika maadili mema,yatakayowafanya kuondokana na
tama ya mafanikio ya haraka,ambayo yamekuwa kichocheo cha kuwepo kwa vitendo
vya rushwa na ufisadi.
Awali Meneja wa Shule za Msingi za Rocken
Hill Academy na Rocken Hill Junior,Ephraim Kabeya,aliiomba jamii kutoa
ushirikiano wa kimalezi kwa vijana na taasisi za kielimu kusudi zimudu kutoa
vijana watakaokuwa viongozi imara na wenye maono ya kuipasha nchi kiuchumi.
Kwa upande wake Meneja wa Benki ya
CRDB Tawi la Shinyanga,Said Pamuyi,aliyekuwa mgeni rasmi katika mahafari hayo,alisema
ili jamii ipate mafanikio ni vyema wazazi na walezi wkawajenga vijana wao
katika maono sahihi ya kiuchumi na kuwasimamia vyema katika maadili.