Saturday, July 29, 2017

DIAMOND AWACHARUKIA WANAOFUATILIA MAHUSIANO YAKE NA ZARI

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO


N
asibu Abdul almaarufu Diamond Platnumz ameamua kuwatolea uvivu kwa kuwaumbua waliokuwa wakisema
kwamba penzi lake za Zari limekufa.


Pia amewajibu wanaotaka mpenzi wake abaki akiwa mnyonge baada ya kupata matatizo ya kufiwa na mama yake mzazi wiki chache zilizopita.

“Kuna vichupi kunuka wanajifanya wanajua sana uchungu wa Misiba ya watu…. Mtoto wa watu katoka katika matatizo mfululizo, anatakiwa apelekwe sehem tulivu apetiwepetiwe adekezwe apate faraja!…sasa kama nyie hamna mabwana wa kuwafanyia hayo, Msijifanye ni Tamaduni na kulazimisha kila mtu awe kama nyie, eti kutwa nzima ajifungie chumbani kulia… Pambaneni na Mahusiano yenu…! Nina siku 5 za kumpetipeti… leo ndio kwanza Ya kwanza 😛.ameandika Diamond Instagram.

Diamond amefikia hatua hiyo baada ya watu kumponda mpenzi wake Zari The Boss Lady, ambaye siku ya jana alikuwa Instalive na mkali huyo wa Eneka wakijiachi kimahaba, hali iliyofanya mitandao ya kijamii kumponda kuwa anaonyesha hana uchungu wa kufiwa na mzazi wake, kazi yake ni kujiendekeza na mapenzi.

Picha zilizozua mijadala mitandaoni ni hizi zifuatazo;

KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI