Wednesday, July 13, 2016

DC NKULU ABARIKI NTOBO KUJENGWA MAKAO MAKUU YA HALMASHAURI MSALALA.

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO


MWITO umetolewa wa kuharakisha  ujenzi wa makao makuu ya Halmashauri ya Msalala wilayani katika Kata ya Ntobo,sambamba na kuiomba Serikali kufanya mchakato wa haraka wa kwa kuanzisha Mamlaka ya Mji Mdogo wa Isaka,ili kusogeza huduma zaidi kwa jamii. 

Mwito huo ulitolewa na baadhi ya wajumbe wa kikao cha Kamati ya Ushauri ya wilaya ya Kahama,kilichoitishwa juzi na Mkuu mpya wa wilaya ya Kahama,Fadhili Nkulu,kubariki Makao Makuu ya Halmashauri ya Msalala kuhamishwa Busangi na kupelekwa Kata ya Ntobo.
 
Mjumbe kutoka Kata ya Isaka,Gavana Ally,alishauri ni vyema Makao hayo yakajengwa haraka baada ya kipindi cha mpito wa marumbano ambayo hayakuwa na tija zaidi ya kuchelewesha maendeleo ya Halmashauri ya Msalala.
 
“…lakini kutokana na makao makuu hayo kuwa mbali kiasi cha kuzifanya Kata zingine kuwa kisiwani,ni vyema basi Serikali ikakamilisha mchakato wa kuanzisha Mamlaka ya mji mdogo wa Isaka,ili kuzidi kusogeza huduma kwa jamii.”Alisema Gavana.
 
Katika Kikao hicho ambacho Nkulu alikitumia kujitambulisha kwa wajumbe ambao ni wadau wa maendeleo wilayani Kahama,wakiwemo na Madiwani wa Halmashauri ya Msalala,kilitumia dakika 27,kupitisha mapendekezo hayo ya kuhamishwa Makao hayo,kama alivyokuwa ameagiza Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga,John Mongela.
 
 
 
Awali Mongela alipokuwa Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga,alipitisha kwa maelekezo makao hayo yajengwe Kata ya Ntobo,badala ya Mega,Segese na Busangi maeneo ambayo yaligubikwa na mvutano wa kisiasa,hali iliyosababisha ujenzi wa makao hayo kukwama kuanzia mwaka 2013,Halmashauri hiyo ilipoanzishwa.
 
Hata hivyo uamuzi wa Mongela,haukufuata taratibu za upatikanaji wa Makao hayo,ikiwemo vikao vya Kamati za Maendeleo ya Kata na kamati ya ushauri ya wilaya licha ya Halmashauri hiyo,kuanza ujenzi kwenye Kata hiyo ya  Ntobo.
 
Kufuatia hali hiyo Nkulu,aliitisha kikao hicho akiwa na lengo la kutia Baraka kisheria ujenzi huo uendelee,ingawa baadhi ya Wajumbe walipitisha uamuzi huo wa kujenga Ntobo kwa madai wamechoshwa na mgogoro huo,kwakuwa wananchi wanahitaji maendeleo,pamoja na eneo hilo kijiografia lipo pembezoni mwa Halmashauri hiyo.
 
Pamoja na Kikao hicho kuwana agenda moja ya Makao Makuu hayo,Nkulu aliwaonya wadau wote kuzingatia muda,uliopangwa wa vikao vyake.Kwakuwa yeye hataki watu wachelewe kwenye vikao na kutumia muda mrefu kujadili agenda moja,alitaka wawe wanawahi kwenye vikao na kutumia muda mfupi kujadili.
 
Kwa upande wake Albart Wakati,mjumbe kutoka Kakola alimtaka Nkulu simu yake ya mkononi iwe wazi wakati wote na akipigiwa awe anapokea haraka,hali ambayo Mkuu huyo wa wilaya alidai atatekeleza hilo na kuwapongeza Madiwani wote na wajumbe wengine waliofika kwa wingi kwenye mkutano huo.
 
Nae James Mhangwa mjumbe kutoka Bugarama,aliwatahadhalisha wataalam  wa ujenzi Katika Halmashauri hiyo,kwamba katika eneo wanaojeng a Makao Makuu hayo,kuimarisha miundo mbinu kutokana na hali halisi ya eneo hilo kujaa mafuriko ya maji wakati wa mvua za masika.
 

KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI