LIFALI BLOG

Categories
  • Home
  • CHAGUA HABARI
    • Business
    • Decoration
    • Entertainment
    • Freelance
    • Inspiration
    • Photoshop
    • Illustration
    • Wallpapers
  • Pages
    • About us
    • Contact us
    • Write for us
    • Advertise
    • Privacy Policy
    • Terms of use
  • Search

Sunday, June 5, 2016

WAFANYAKAZI ACACIA BULYANHULU WAADHIMISHA SIKU YA MAZINGIRA KWA KUFANYA USAFI KIJIJINI

By   21:20   No comments:
BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO


 
WAFANYAKAZI wa Mgodi wa Dhahabu Wa Acacia Bulyanhulu wamesherehekea siku ya Mazingira Duniani kwa kufanya kazi ya kusafisha mazingira katika Kijiji cha Ilogi kilichopo katika Halmashauri ya Msalala Wilaya ya Kahama Mkoani Shinyanga.

 

Akizungumza wakati wa zoezi la usafi kijijini hapo Afisa Mtendaji wa Kijiji cha Ilogi Christopher Galila amesema hatua ya wafanyakazi kusafisha mazingira ya kijiji ni funzo muhimu kwa wananchi wengine na kusema kwamba uchafuzi wa mazingira hautavumiliwa katika maeneo yoyote kijijini humo.

 

“Pamoja na kutusaidia kusafisha hii leo meneo mbalimbali kwenye vizimba vya uchafu ambavyo baadhi vimekuwa na taka kwa muda mrefu pamoja na soko letu, Mgodi umetupatia mapipa kumi na tano ya kutupia taka ambayo yatatusaidia katika siku za usafi za kila juma, kwani kijiji chetu kina utaratibu wa kukusanya na kukagua usafi wa mazingira kila siku ya Jumamosi.”

 

Naye Kaimu Meneja wa Ufanisi wa Mgodi wa Bulyanhulu Bwana Onesmo Kabeho amesema timu ya wafanyakazi imefurahi mwitikio wa wananchi walioungana na wafanyakazi kusafisha mitaa, mitaro, vizimba vya taka na soko la kijiji.

 

“Sisi leo tumefurahi sana kung’arisha maeneo mbalimbali kijijini hapa kwa kuondoa kero ya uchafu ambao ni hatari kwa mazingira, tunatoa mwito kwa wanajamii wote kutunza mazingira kwa njia mbalimbali ikiwemo kudhibiti takataka hasa plastic ili watoto wetu na vizazi vijavyo visipate athari ya uchafuzi wa mazingira wa sasa”.
 
Wafanyakazi wa Bulyanhulu Wakikusanya uchafu kwenye mitaro katika kijiji cha Ilogi.
Mfanyakazi wa Mgodi wa Bulyanhulu Dennis Cowan akiwa amebeba Pipa la Taka wakati wa zoezi la kusafisha mitaa.
Usafi ukiendelea katika Mazingira ya Soko la asili katika kijiji cha Ilogi.
 
Wauzaji wa Mbogamboga wakifurahia zoezi la usafi Sokoni
 
 
 
 
Kaimu Meneja wa Ufanisi wa Mgodi wa Bulyanhulu Bwana Onesmo Kabeho akikabidhi mapipa 15 ya kutupia takataka kwa uongozi wa kijiji cha Ilogi.
 
Chanzo cha Habari ni Afisa Habari wa Mgodi wa Dhahabu wa Bulyanhulu ;-Mary Lupamba. 

KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI
  • Facebook
  • Twitter
  • Google
  • Whatsapp
  • More
  • Pinterest Linkedin Digg This Reddit StumbleU Delicious

    Newer Post Older Post

    IDADI YA WASOMAJI WETU

    Habari Kali Zaidi

    • MADHARA YA MATUMIZI YA MUDA MREFU WA MADAWA YA MAJIRA
      PAMOJA na Serikali kuwa na sera ya uzazi wa mpango na kuridhia matumizi ya vidonge au sindano za majira ama njia za njiti ili kuzuia kupata ...
    • MAJINA NA MAJIMBO YAO WABUNGE WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
      TANZANIA imefanya Uchaguzi Mkuu wa Rais,Wabunge na Madiwani Oktoba 25,mwaka huu. Na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania linata raj ...
    • LEMBELI,MGEJA WAITESA CCM SHINYANGA.
      M bunge wa zamani wa Jimbo la Kahama,James Lembeli, na aliyekuwa Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa S...
    • SHINYANGA YAPIGA MARUFUKU BIASHARA YA NGONO
      YUPO kikazi zaidi MKUU wa Mkoa wa Shinyanga;Ally Nassoro Rufunga,amepiga marufuku biashara ya ngono inayoshika kasi katika Halmas...
    • UTANDAWAZI UMEATHIRI MILA ZETU WATANZANIA
      Nchini Tanzania kuna makabila mengi ambapo baina yake,kuna utani wa jadi miongoni mwao.Utani huu wa jadi upo karne na karne kabla hata ...

    MAKTABA YETU

    CHAGUA HABARI

    • Ali Lityawi na Hassani Alli
    • habari
    • HABARI ZA KIMATAIFA
    • HABARI ZA KITAIFA
    • habari za michezo na burudani
    • HABARI ZA MICHEZO NA UTAMADUNI
    • HABARI ZA NYUMBANI
    • magazeti
    • Na Ali Lityawi
    © Copyright 2016 LIFALI BLOG. Designed by Bloggertheme9. Powered by Blogger.