Wednesday, June 1, 2016

ACACIA KUENDELEZA ELIMU YA MADINI NCHINI.

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO


 MGODI wa dhahabu wa Bulyanhulu(BGML)unaomilikiwa na Kampuni ya ACACIA,utaendelea kutoa fursa ya mafunzo kwa vitendo mgodini hapo,kwa vijana wanaosoma elimu ya madini katika Chuo Kikuu cha Tanzania ili kuendeleza sekta ya madini nchini.

Kauli hiyo imetolewa hivi karibuni na Meneja Ufanisi na Uendelevu wa Mgodi huo,Elias Kasitila,alipokuwa akikaribisha kundi la 42 la Wanachuo wa mwaka wa tatu kutoka Chuo Kikuu cha Dar Es Salaam,wanaochukua mafunzo ya madini walioambatana na baadhi ya Wahadhiri wao,ambapo alisema mgodi upo tayari kutoa kipaumbele ya mafunzo kwa vitendo kwa vijana wanaochukua elimu hiyo kutoka Chuo Kikuu.

 Kasitila alisema Kampuni ya Madini ya Acacia imejipanga kuendeleza sekta ya madini nchini kwa kusaidizana na Serikali kwa kutoa fursa kwa wasomi wanaosomea madini kufika kujifunza kwa vitendo hatua itakayosaidia Taifa la Tanzania kupata Wataalamu wenye ujuzi stahiki wa madini.

"....kampuni yetu ina nia ya kusaidia sekta ya madini nchini,kwa kuchangia katika mchakato wa kuwaandaa kwa kuwapatia mafunzo ya vitendo wasomi tunaotarajia kuwa wahandisi wajao wa madini kupitia mpango,huu endelevu  wa wanachuo kujipatia elimu kwa vitendo hapa mgodini."Alisema Kasitila.

Nae Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar Es Salaam,Geofrey William,alisema tangu makubaliano baina ya Mgodi na UDSM kufanyika mwaka 2008,juu ya udhamini wa mafunzo kwa vitendo unaofanywa na mwekezaji huyo,umesaidia kuleta ufanisi kwa vijana wanaochukua mafunzo ya masuala ya madini.

Akitoa shukrani kwa mgodi uliotoa fursa ya kuutembelea ili kujionea shughuli mbalimbali zifanyikazo mgodini,Mhadhiri Dk.Richard Katemi,alivutiwa na utaratibu wa kiusalama uliowekwa mgodini unaowawezesha watumishi,kwenda kazini na kurejea majumbani salama.

Aidha alipongeza hatua ya Mgodi kutoa fursa kwa wasomi wa Chuo Kikuu cha Dar Es Salaam,wanaochukua mafunzo ya masuala ya madini kupata mafunzo ya vitendo ambayo yamekuwa msaada mkubwa wa kufahamu kwa kina walichokuwa wakijifunza chuoni.  

“Ni kweli kwamba,sisi ni kawaida yetu kuwafundisha wanachuo kwa nadharia,ziara kama hii husaidia kupata uelewa zaidi,na zaidi husaidia kwa wanachuo kuziba pengo kwa kupata mafunzo kwa vitendo,ambayo huwafanya kujifunza mengi yanayowaongezea tija katika uwajibikaji wenye ufanisi wa shughuli za madini pindi wanapokuwa katika ajira,”alisema Dk.Katemi.

Kwa upande wake Mwanachuo,Bahati Moshally alisema ziara hiyo ya mafunzo,inasaidia kuongea ujuzi baada ya kufanikiwa kupata mafunzo ya nadharia yanayokuwa muongozo wa kufanikisha mafunzo ya vitendo,ambayo yanasaidia kufahamu zaidi masuala ya usalama migodini mbali na utekelezaji wa uchimbaji unavyofanyika.

“Kwa tunayonufaika kwa vitendo,shukrani zetu tunazitoa kwa uongozi wa Mgodi wa Acacia na Chuo Kikuu chetu,kwa kujinga fursa hii adhimu kwetu wanachuo,”alisema Moshally.

Ziara hiyo ni ya nane kwa wanachuo kutoka Chuo Kikuu cha Dar Es Salaam,ambayo hufanyika mara moja kila mwaka,na tayari zaidi ya wanachuo Elfu Moja wameishanufaika kwa kupata mafunzo ya vitendo.

Chanzo cha Habari:Mary Lupamba.

KUNDI la Wanachuo wakiwa na wakufunzi wao wakianza ziara ya kutembelea mgodi kujionea shughuli za uchimbaji wa dhahabu.
 

 MENEJA wa Ufanisi na Uendelevu wa Mgodi wa Dhahabu wa Bulyanhulu,Elias Kasitila akizungumza na Wanachuo wa UDSM,mara walipomaliza kutembelea chini ya ardhi kunakofanyika uchimbaji wa ardhi. 



MMMMMMMMMMMMMMMMMMMMMMMAdd caption
Add captionkundi la Chuo Kikuu cha Dar es salaam Wanafunzi waliotembelea Bulyanhulu Gold Mine Jana viongozi wa mgodi chini ya ardhi.
Bulyanhulu Gold Mine Shirika Ufanisi na Sustainability Meneja Elias Kasitila Akizungumza na UDSM Wanafunzi baada ya ziara yao katika Bulyanhulu Gold Mine Underground
 .

KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI