Wednesday, April 13, 2016

WATANZANIA WATAKIWA KUCHANGAMKIA FURSA ZA KIBIASHARA AFRIKA MASHARIKI

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO




MWITO umetolewa kwa Wananchi wa Tanzania,kuchangamkia fursa za kibiashara zilizopo katika nchi za Afrika Mashariki,ili kujiletea maendeleo na kukuza uchumi wa nchi, kutokana na kuwepo makubaliano,yaliyofikiwa na kuwapa wananchi wa nchi za Afrika Mashariki kufanya biashara kwa uhuru.

Mbunge wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Makongoro Nyerere,alitoa wito huo wakati akizungumza na waandishi wa habari katika ukumbi wa idara ya Habari Maelezo, jijini Dar es Salaam na kusema kuwa nchi za Afrika Mashariki zinashirikiana kwa mambo mbalimbali ikiwepo umoja wa forodha, soko la pamoja, umoja wa fedha na shirikisho wa kisiasa.

Akiongea na waandishi wa habari hao alitumia fursa hiyo kutoa wito huo kwa kubainisha kupitia makubaliano hayo Watanzania wana nafasi ya kwenda kufanya biashara katika nchi zingine bila kuzuiliwa na hivyo kuwa na nafasi ya kusambaza bishaa zao katika nchi zote wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Alifafanua kwamba ni wakati wa Wafanyabiashara wa Watanzania kuchangamkia nafasi zilizopo za kufanya baishara kwa nchi za Afrika Mashariki, japo alikiri kuwa vikwazo vilivyopo kwa sasa ni juu ya wananchi wengi wa Afrika Mashariki,hususani Watanzania kutokuwa na uelewa wa kutosha juu ya jambo hilo.

Hata hivyo alibainisha kwa upande wa Tanzania wamejipanga kuhakikisha fursa hizo za kibiashara zinatumiwa vyema hasa baada ya kubaini changamoto hiyo ya wananchi wengi kutokufahamu nafasi hiyo, wabunge wa Jumuiya ya Afrika Mashariki wa Tanzania wataendesha programu ya kuwaelimisha Watanzania jinsi wanavyoweza kunufaika na ushirikiano huo.

Alisema programu hiyo ilianza Aprili 4 na itafanyika hadi Aprili, 23 ambapo kwa kuanza wamepanga kukutana na Kamati za Bunge, Taasisi za Elimu ya Juu, vyombo vya habari, kutembelea soko la Kariakoo na soko la Samaki la Feri.

Pia Nyerere amewataka Watanzania kuwa na mazoea ya kutafuta taarifa mbalimbali kupitia mitandao kwani kwa kufanya hivyo wanaweza kukutana na fursa nyingi ambazo hawakuwa wakizifahamu awali.

KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI