Wednesday, April 13, 2016

WANAHISA CRDB WAOMBA KUGHARAMIWA VIKAO VYA KITAIFA

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO

BAADHI ya wana hisa katika Benki ya CRDB,wanaomiliki hisa chache Wilayani Kahama,wameiomba Benki hiyo kuwawezesha   kuhudhuria vikao mbalimbali vya kitaifa vinavyoandaliwa na taasisi hiyo,kwakuwa wana mchango katika kukua kwa taasisi hiyo, badala ya wao kujitegemea kwa sasa.
Ombi hilo lilitolewa na Wanahisa hao wa Benki ya CRDB Tawi la Kahama,katika kikao chao cha siku moja cha Wanahisa,ambapo mmoja wa Wanahisa hao; Marco Nzela alisema kuwa wamekuwa wakishindwa kuhudhuria vikao vikuu hivyo jambo linalosababisha kushindwa kuwasilisha changamoto zao na kusababisha kupitwa na mambo mengi ya maana.
Alisema kuwa kama Benki hiyo ya CRDB ingekuwa inagharamikia wanahisa wake katika vikao mbalimbali vinavyowahusu vya kitaifa kungekuwa na Wanahisa wengi ambao wangekuwa wakihudhuria na hivyo kutoka na elimu zaidi itakayowasaidia katika kukuza mitaji yao.
“Kwa sasa Wanahisa tunajigharamia wenyewe katika vikao hali ambayo kwa sisi Wanahisa wenye hisa ndogo, inakuwa ni vigumu kuhudhuria kutokana na kukosa fedha na hivyo kupelekea kutopata Elimu ya kutosha katika fani ya biashara kwa ujumla”, Alisema Marco Nzela Mwanahisa wa Benki ya CRDB Kahama.
Aidha pamoja na mambo mengine Wanahisa hao waliuomba uongozi wa Benki ya Benki ya CRDB Nchini kuhakikisha inabadili sehemu ya kufanyia mikutano yake ya Wanahisa badaka ya kuweka katika Mkoa wa Arusha kila mwaka hali ambayo inakuwa vigumu kwa wale wanaotoka katika mikoa ya pembezoni kuhudhuria.
Katika kikao hicho cha umma na Wanahisa wa Benki ya CRDB ambapo kulitolewa mada mbalimbali kutoka kwa mtaalamu wa Benki ya CRDB ambaye pia ni Mwanasheria Charles Lauwa Wanahisa hao pia walitakiwa kufungua akaunti ya Busara ili kuweza kuongeza amana zao.
Lauwo alisema kuwa  kati ya Wanahisa 11,500 waliolipwa gawio  kupitia Benki yaCRDB  kwa mwaka 2014 kupitia akaunti za Benki, 11881 walilipwa klupitia katika akaunti ya Busara huku waliobaki wakilipwa kupitia akaunti nyingine.
Aidha Mkufunzi alisema kuwa  hata kama unakuwa na hisa katika Makampuni mengine unaweza pia kutumia  akaunti hiyo  ya Busara  ambayo kwa ujumla inashirikisha watu wote na pia inamtambulisha mteja katika neo husika aliloweka hisa zake.
Hata hivyo Lauwo alisema kuwa akaunti hiyo ya Busara hufunguliwa  kwa fedha za kitanzania na kuongeza kuwa  amana unazotakiwa kuweka katika akaunti hiyo  ni kuanzia kiasi cha shilingi 200,000 huku kiasi cha riba yake ikiwa ni asilimia tatu  kwa kwaka.
Hata hivyo Lauwo alisema kuwa ili kuweza kufungua akaunti ya Busara lazima uweze kukidhi vigezo vyake kama vile  vya kuwa miliki  wa hisa  katika Kampuni  iliyoorodheshwa katika sko la his alas Dar es Salaam (DSE) na kuongeza kuwa pindi ukifungua akaunti hiyo amana yako itaingia moja kwa moja.

KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI