Tuesday, April 19, 2016

RC MWANZA ATOA SIKU SABA KUREJESHWA KIWANJA KILICHODHURUMIWA

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO



MKUU wa mkoa wa Mwanza,John Mongella, ametoa wiki moja kwa  uongozi wa Jiji la Mwanza, kuhakikisha linakabidhi kiwanja namba 28-A kilichopo katika eneo la Bugando,kwa mmiliki wake halali,Justine Eminoga, ambacho amekuwa akikidai kwa kipindi cha miaka sita baada ya kupokwa na mfanyabiashara wa Jijini humo.

Hatua hiyo ya Mkuu wa Mkoa kutoa agizo hilo imefikia,mara baada yakupokea malalamiko kutoka kwa Justine ambaye alifika katika Jiji la Mwanza kwa ajili kufatilia suala lake hilo.

 Akitoa malalamiko yake mbele ya mkuu huyo wa mkoa,Justine alidai kudhurumiwa kiwanja hicho na mfanyabiashara aliyemtaja kwa jina Shanif Mansour ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Kwimba.

Katika hatua nyingine mkuu huyo wa mkoa ametoa siku saba kwa halmashauri za mkoa wa Mwanza kuhakikisha wanakamilisha zoezi la kuhakiki  watumishi, ili kubaini endapo kuna watumishi hewa waliosalia katika zoezi la awali, zoezi la sasa ambalo linasimamiwa na Ofisi ya katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza kwa kamati maalumu zilizo undwa na mkuu wa Mkoa huo.
 
Akiwa katika ziara hiyo mkuu huyo wa mkoa aliagiza kukamatwa kwa Afisa Utumishi msaidizi wa jiji la Mwanza Henry Sedetale, ambaye alisaidia watumishi hewa watano kuchukua mikopo ya zaidi ya Mil.90 kutoka katika benki tofauti tofauti, hata hivyo taarifa kutoka  Taasisi yakupambana na kuzuia rushwa mkoani Mwanza  iliyotolewa wakati wa kikao hicho na mkuu wa Takukuru mkoani humo, ilisema mtuhumiwa huyo tayari alikuwa ametiwa nguvuni na taasisi hiyo kwa mahojiano zaidi.

Mkuu wa mkoa wa Mwanza yupo katika ziara kujitambulisha katika mkoa huo na hii ikiwa ni Wilaya yake ya tatu mara baada yakutembelea wilaya za Misungwi na Magu hapo awali.

KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI