WAJUMBE
wa Kamati ya Kudumu ya Bunge na Sheria wamepewa rai ya kushikamana na Serikali
katika kuhakikisha kuwa maboresho ya Sheria ya Vyama vya Siasa ya mwaka1992 na
Sheria ya gharama za uchaguzi ya mwaka 2010 yanafanyika ili kuondoa utata na
migongano ya utekelezaji wa masuala ya siasa nchini.
![]() |
Waziri wa Sera, Bunge, Kazi , Vijana, Ajira na Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama akijibu hoja |
Hayo
yamesemwa na Waziri wa Sera, Bunge, Kazi , Vijana, Ajira na Ulemavu Mhe.
Jenista Mhagama wakati akijibu swali kutoka kwa wajumbe kwenye kikao cha kamati
ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria cha kupitisha bajeti ya Ofisi ya Msajili
wa Vyama vya Siasa kilichofanyika Leo katika ukumbi wa Saadan wa Mwalimu
Nyerere Jijini dar es salaam ambao walihoji uhalisia wa utekelezaji wa sheria
zililizopo sasa.
![]() |
Kikao cha kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria |
Wajumbe
hao walihoji utitiri wa vyama vingi nchini ambavyo miaka nenda rudi havina
madiwani wala wabunge na vingine kutoshiriki katika chaguzi . Wajumbe pia
walihoji gharama ndogo za usajili wa vyama vya siasa ukilinganisha na hali ya
maisha iliyopo kwa sasa.
![]() |
![]() Katibu kiongozi wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria,Angelina Sanga, |
Jambo
lingine ambalo wajumbe wamehoji ni nafasi ya Msajili wa Vyama vya Siasa katika
kushughulikia migogoro ya kisiasa ndani na nje ya Vyama vya Siasa na
ushirikishwaji wa wanawake katika maamuzi ndani ya vyama vya siasa.
![]() |
Mjumbe wa kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria, Mhe Richard Ndassa akiwasilisha hoja |
Akijibu
hoja hizo Mhe Mhagama amesisitiza kuwa maboresho ya Sheria ya Vyama vya Siasa
na Sheria ya Gharama za uchaguzi ndio njia pekee itakayompa meno Msajili wa
Vyama vya Siasa nchini katika kutekeleza majukumu yake ipasavyo.
“Sheria
tulizonayo ndio inatoa mwanya wa haya yote haya na ndio maana Serikali kwa sasa
inaendelea na taratibu za kuboresha sheria hizi, tayari Ofisi ya Msajili wa
Vyama vya siasa ameshawasilisha mapendekezo ya maboresho ya Sheria ya Vyama vya
Sasa na Sheria ya gharama za uchaguzi na sisi tumeridhia , tunasubiri tu bunge
kujadili ili ziweze kutumika”alisisitiza mhe Mhagama.
CHANZO
CHA HABARI NI KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI OFISI YA MSAJILI WA
VYAMA VYA SIASA
KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI