Friday, November 27, 2015

CHADEMA,FAMILIA YA MAWAZO YASHINDA KESI

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO




HATIMAYE  Chama cha Demokrasia na Maendeleo “CHADEMA” na familia ya Mwenyekiti wa CHADEMA Geita Alphonce Mawazo wameshinda kesi
dhidi ya Jeshi la Polisi lililozuia mwenyekiti huyo,asiagwe  jijini Mwanza baada ya kuuawa kinyama kwa kukatwa mapanga.

 Taarifa kutoka Mahakama kuu
Kanda ya Mwanza zinaarifu kuwa Familia ya Alphonce Mawazo na Chadema  wameruhusiwa kuendelea na taratibu za kuaga mwili wa marehemu na kuzika, huku Polisi wakitakiwa kutoa ulinzi kama ilivyo wajibu wao kwa kuzingatia mipaka ya kazi yao.

Akitoa hukumu hiyo,Jaji Lameck Mlacha,alisema Mahakama Kuu Jijini Mwanza  imetoa ruhusa mwili wa Alphonce Mawazo kuagwa jijini Mwanza na kisha kuuzika mwili wa mpendwa wao huyo ila wafuate tu utaratibu,huku ukiliagiza Jeshi la Polisi kutoa Ulinzi siku hiyo lakini Ulinzi huo usivuke mipaka.

Kulikuwepo sintofahamu juu ya hatma ya kuuzika mwili wa aliyekuwa Mwenyekiti wa CHADEMA, Geita   Mawazo baada ya kutokea kwa mvutano kati ya UKAWA na Jeshi la Polisi. Ambapo Jeshi la polisi lilitoa amri kuwa Mawazo asiagwe Mwanza kwa kuwa kuna hofu ya kipindupindu,huku familia kwa kushirikiana na UKAWA ikipinga amri hiyo,ambayo imetupiliwa mbali na Mahakama hiyo. 
  

Katika kesi hiyo Viongozi mbalimbali wa CHADEMA akiwemo Mbunge na Mwenyekiti wa Chama hicho, Freeman Mbowe walikuwa wakiongoza wafuasi wa UKAWA waliokuwa wakihudhuria mwenendo wa kesi hiyo,ambapo upande wa Mashitaka uliongozwa na Mwanasheria wa Chama hicho, John Mallya.

Familia ya Marehemu Alphonce Mawazo na CHADEMA walifungua kesi hiyo kuomba tafsri ya mahakama, dhidi ya  mapingamizi yaliyowekwa na RPC wa Mwanza na Mwanasheria Mkuu wa Serikali,kupiga marufuku mikusanyiko ya kuuaga mwili wa marehemu Alphonce Mawazo.

KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI