Monday, November 3, 2014

MILIONI 36 KUKAMILISHA MAABARA YA KATA KAHAMA

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO



JUMLA ya Shilingi Milioni 36 zinatarajia kukamilisha vyumba vitatu vya maabara na ofisi tatu katika shule ya sekondari Bugisha iliyopo Kata ya Mondo wilaya ya Kahama mkoani Shinyanga.
 
Hayo yalisemwa na Diwani wa Kata ya Bugisha Said Hamad, wakati akiongea na Gazeti tando hili katika shule hiyo ambapo ujenzi huo unaendelea. 

Alisema maabara hiyo inajengwa kwa nguvu za wananchi na itakapofika mwezi Desemba mwaka huu ujenzi wa maabara hizo  utakuwa umekamilika kadri ya maagizo ya serikali. 

Hamadi aliwaomba wananchi wa kata hiyo kuendelea kutoa ushirikiano ili kukamilisha agizo la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Jakaya Mrisho Kikwete wa shule zote za kata kuwa na maabara. 

Aidha Said aliipongeza Halmashauri ya Mji kwa kutoa tofali 4,000 kwa kila Kata ili kuweza kukamilisha ujenzi huo ambapo mchango huo umeongeza  nguvu zaidi kwa wananchi na kuendelea kuwa na imani na serikali iliyopo madarakani.

KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI