Sunday, October 19, 2014

WATANI WA JADI NCHINI WATOSHANA NGUVU MANYIKA JUNIOR SHUJAA

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO

MSHAMBULIAJI Elius Maguli wa Simba akiwatoka mabeki wa Yanga.

WATANI wa jadi na timu kongwe nchini Yanga na Simba zimetoshana nguvu katika pambano kali la Ligi kuu Tanzania Bara,lililochezwa uwanja wa Taifa Jijini Dar Es Salaam.

 MASHABIKI wa Yanga wakifuatilia pambano


Katika pambano hilo ambalo macho ya washabiki yalikuwa kwa washambuliaji Denilson Jaja wa Yanga na Emmanuel Okwi wa Simba kuwa watazisaidia nini timu zao,lilimalizika pasipo kufungana huku kipa wa Simba Peter Manyika akionyesha umahiri mkubwa katika kulinda lango.

HOFU;Ilikuwa kosakosa langoni mwao


 Manyika ambaye Yanga walidai akiketi langoni watammiminia mvua ya magoli,alionyesha utulivu wa hali ya juu na kuisaidia timu yake isipachikwe bao.

 Kinda huyo alianza kuonyesha umahiri wake wa kulinda lango mnamo  Dakika ya 13,baada ya  Jaja kutuliza mpira katikati ya mabeki ya Simba kisha kuachia shuti kiufundi, lakini Manyika alilidaka shuti hilo kwa umaridadi mkubwa.

 AKINA Dada hawa ni mashabiki kindakindaki wa Yanga

Mnamo Dakika ya 17 Okwi alitengenezewa mpira mzuri na Shabalala lakini shuti kali lilitoka nje kidogo.Na Yanga walijibu shambulizi hilo sekunde 36 baadaye,lakini Manyika JR anafanya kazi kubwa kwa kutoka na kulidaka shuti la Coutinho.



Dakika ya 18, Okwi aliyeonekana mwiba kwa mabeki wa Yanga alituliza mpira kifuani na kumzidi maarifa Juma Abdul,akiwa mbele ya Cannavaro,alimhadaa na kuachia kombora lililotoka juu kidogo ya lango la Yanga.
 

 MASHABIKI wa Yanga wakiilaki timu yao


Mnamo Dakika ya 72,Manyika alifanya kazi ya ziada tena baada ya kutoka na kuuwahi mpira aliokuwa nao Mrisho Ngassa aliyefaulu kuingia eneo la hatari baada ya kupokea pasi safi ya Coutinho.

Kipa kinda huyo wa Simba alizidi kudhihirisha umahiri wake mnamo Dakika ya 77,baada ya kuokoa shuti la Coutinho aliyekuwa peke yake akimtazama.

Mshambuliaji wa Simba Haruna Chanongo mnamo Dakika ya 84, alifanikiwa kuisambaraisha ngome ya Yanga lakini shuti lake kali lilipaa juu ya lango la Yanga.

MNAZI wa Simba wa Jacob Steven "JB" na Shabiki wa Yanga Irene Uwoya wakifanyiana ufyosi kabla ya pambano.



Katika pambano hilo Yanga waliokuwa mwenyeji wa mchezo huo,walipata kona nne na Simba kona tatu.

HUKO Mtwara, Ndanda FC imeonja utamu wa kufungwa nyumbani baada ya kuchapwa mabao 3-1 na JKT Ruvu.
Ndanda imefungwa mabao hayo ikiwa kwenye Uwanja wa Nangwanda Sijaona mjini Mtwara.

Mabao ya JKT Ruvu yalifungwa na Juma Ndeule, Abrahman Mussa na Thomas Matayo.

 Mjini Morogoro, Polisi Moro na Mtibwa Sugar zimemaliza dakika 90 bila ya kufungana.


Nako Jijini Mbeya bao la nahodha Aggrey Morris ndiyo ‘sumu’ iliyoimaliza Mbeya City huku Azam FC ikiibuka na ushindi wa bao 1-0.Na kuifanya Mbeya City kuendelea kuwa wateja wa wana lambamba.

Licha ya kuwa nyumbani, Mbeya City ilishindwa kuizuia Azam FC baada ya bao hilo moja la Morris lililofungwa kwa mkwaju wa adhabu baada ya Kipre Tchetche kuangushwa nje ya 18.

Mara ya mwisho zimekutaka kwenye uwanja huo ilikuwa ni mechi ya kufunga msimu na Azam FC ikashinda na kubeba ubingwa.

Mjini Tanga, Coastal Union imeshinda kwa mabao 2-0 dhidi ya Mgambo.

KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI