Monday, October 20, 2014

TRAFIKI WAONYWA KUPOKEA RUSHWA ILI KUDHIBITI AJALI NCHINI

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO

DCP Mohammed Mpinga


JESHI la polisi nchini limewaonya askari wa kitengo cha usalama barabarani kuacha vitendo vya kupokea rushwa ili kuzuia ajali za barabarani zinazoendelea kupoteza uhai wa watu wasio na hatia huku zikiwaachia wengine ulemavu wa maaisha.


Kauli hiyo ilitolewa  mjini Dodoma na Kamanda wa Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani nchini,DCP Mohammed Mpinga alipowahutubia wakurugenzi na mameneja wa Radio Jamii nchini kwenye mkutano wa siku nne na wadau mbalimbali wanaoshirikiana nao kimawasiliano.

Mpinga alisema, jumla ya watu 4,000 wanapoteza maisha kila mwaka kwa ajali za barabarani ambazo Chanzo chake kikubwa ni makosa ya kibinadamu kama uzembe wa madereva, ulevi, mwendo kasi, kutozingatia sheria na uchovu wa safari.

Aliendelea kusema kuwa sababu nyingine ni matumizi ya vyombo vya moto pasipo kupata mafunzo, huku ukaguzi na usimamizi unaofanywa na askari wa usalama barabarani ukugubikwa na wimbi la rushwa.

Mpinga aliziomba radio za jamii kushiriki kwa kina katika kuwaelimisha wananchi kwamba wanayo nafasi kubwa ndani ya jamii kukomesha ajali hizo kwa kuhakikisha makondakta hawashiriki kutoa rushwa kwa askari wakati wanapokuwa wamekamatwa na makosa.

Alisema  jeshi la polisi limekwishatoa maelekezo dhidi ya askari kumchukua kondakta pembeni na kumtoza rushwa hali ambayo ni sawa na kuuza maisha ya abiria wanaosafiri na gari husika.

Mpinga alisisitiza kuwa adhabu anayotozwa kondakta inatakiwa iandikwe mbele ya abiria na wala siyo kweye gari la askali, kivuli wanachokuwa wanapumzika wakiwa kazini, na wala siyo kuwekwa kwenye nyaraka za gari mithili ya kwamba zinakaguliwa.

Kwa upande wake mwenyekiti wa mtandao wa radio jamii nchini COMNETA, Joseph Sekiku alimthibitishia Mpinga kwamba, radio hizo zinazowafikia zaidi ya wasikilizaji milioni 16 nchini, zimekubali kushirikiana na ofisi yake katika kutoa elimu ya usalama barabarani.

Nao Wajumbe 48 waliohudhuria kikao hicho wamemwomba mpinga kutoa ushirikano wa kina pale ofisi yake inapohitajika na kuchukua hatua mwafaka kwa matukio yatakayotolewa kwa vielelezo makini dhidi ya watu wanaorudisha nyuma juhudi hizo.

KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI