Tuesday, October 21, 2014

POLISI ARUSHA WAMUUA MTUHUMIWA WA UGAIDI

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO

 SACP Liberatus Sabas


JESHI la Polisi mkoa wa Arusha limefanikiwa kumuua kwa kumpiga risasi Yahaya Hassani Omary anayetuhumiwa kuwa ndiye Kinara wa  matukio ya
ulipuaji wa mabomu na umwagiaji tindikali viongozi wa dini.
 

 Kamanda wa Polisi mkoani Arusha,SACP Liberatus Sabas Alithibitisha kutokea kwa tukio hilo  Oktoba 19 mwaka huu majira ya saa tano na nusu  katika barabara ya Babati mkoani Arusha wakati mtuhumiwa akijaribu kuwakimbia polisi.

Alisema mtuhumiwa huyo wa ugaidi mara baada ya kutafutwa kwa muda mrefu alikamatwa na kushikiliwa wiki mbili zilizopita  mkoani Morogoro   na aliuawa wakati akipelekwa wilayani Kondoa mkoani Dodoma  kwa ajili ya kwenda kuonyesha sehemu ambazo alikuwa ameficha mabomu mengine.

Kamanda Sabas alisema Mtuhumiwa huyo alikuwa anasakwa kwa muda mrefu bila mafanikio kwani alikuwa hakai sehemu moja ila jeshi la polisi huko mkoani Morogoro lilimkamata,na baada ya kufanyiwa mahojiano alisema ameficha mabomu mengine huko Kondoa.

“Wakati akipelekwa kuonyesha alipoyahifadhi,ndipo alipotumia mbinu zake ambazo amefundishwa za ugaidi kwa kupiga judo na kutaka kuwakimbia askari ndipo akapigwa risasi mbili"alisema Sabas.

Aidha Kamanda Sabas alitoa wito kwa wananchi kuendelea kuwafichua waovu  ili kuweza kuteketeza matukio ya uhalifu.

KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI