BINGWA wa Soka Uingereza msimu wa
mwaka 2016/2017,timu ya Chelsea,itaanza kampeni ya kutetea taji la Ligi Kuu ya
England kwa mechi ya nyumbani dhidi ya
Burnley,katika mchezo utakaochezwa mwisho wa wiki,tarehe 12-13 Agosti.mwaka huu.
Burnley,katika mchezo utakaochezwa mwisho wa wiki,tarehe 12-13 Agosti.mwaka huu.
Mechi ya kwanza ya Spurs katika uwanja
wa Wembley itakuwa dhidi ya mabingwa wa Antonio Conte wikendi ya pili ya msimu.
Mechi za mwisho za ligi zitachezwa
Jumapili 13 Mei, 2018 wiki moja mapema kuliko msimu uliopita kutokana na
fainali za Kombe la Dunia ambazo zitaanza Urusi 14 Juni.
Ratiba ya mechi za Kombe la Ligi ya
England itatolewa 21 Juni nayo ya mechi za Scotland siku mbili baadaye.
Mechi za ufunguzi Jumamosi, 12
Agosti, 2017
Arsenal v
Leicester City
Brighton v
Manchester City
Chelsea v
Burnley
Crystal Palace
v Huddersfield Town
Everton v
Stoke City
Manchester
United v West Ham United
Newcastle
United v Tottenham Hotspur
Southampton v
Swansea City
Watford v
Liverpool
West Bromwich
Albion v AFC Bournemouth
Aidha kumekuwa na mashaka kuhusu uwezo
wa Tottenham kutamba Wembley ikizingatia matokeo yao katika uwanja huo Ligi ya
Klabu Bingwa Ulaya msimu uliopita.
Vijana hao wa Mauricio Pochettino
watakuwa an kibarua kigumu mechi yao ya kwanza uwanja huo wao wa muda.
Mara ya mwisho walipokuwa Wembley,
ilikuwa nusu fainali Kombe la FA msimu uliopita ambapo walilazwa 4-2 na
Chelsea.
Lakini wiki za kwanza huenda zikawa
ngumu kwa mabingwa watetezi pia, huku Chelsea wakiwa wenyeji wa Everton (26
Agosti), wawatembelee washindi wa 2015-16 Leicester baada ya mapumziko ya
kimataifa na kisha wawe wenyeji wa Arsenal (16 Septemba).
Vijana wa Arsene Wenger watakuwa na
nafasi ya kuonyesha uwezo wao msimu ujao watakapozuru Anfield kucheza na
Liverpool wiki ya tatu.
Mechi zitakazofuata Liverpool watazuru
Etihad Stadium kukabiliana na Manchester City.
Katika hiyo, klabu zitacheza mechi nne
katika kipindi cha siku sita wakati wa Krismasi na Mwaka Mpya, kwa jumla
zitakuwa mechi nane kuanzia 2 Desemba hadi 1 Januari.
Jumamosi, 19 Agosti, 2017
AFC
Bournemouth v Watford
Burnley v West
Bromwich Albion
Huddersfield
Town v Newcastle United
Leicester City
v Brighton
Liverpool v
Crystal Palace
Manchester
City v Everton
Stoke City v
Arsenal
Swansea City v
Manchester United
Tottenham
Hotspur v Chelsea
West Ham
United v Southampton
Jumamosi, 26 Agosti, 2017
AFC
Bournemouth v Manchester City
Chelsea v
Everton
Crystal Palace
v Swansea City
Huddersfield
Town v Southampton
Liverpool v
Arsenal
Manchester
United v Leicester City
Newcastle
United v West Ham United
Tottenham
Hotspur v Burnley
Watford v
Brighton
West Bromwich
Albion
KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI