Wednesday, June 14, 2017

VIWANJA 100 KAHAMA VYADAIWA KUGAWIWA KIMAKOSA

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO

IMEELEZWA zaidi ya viwanja 100, katika  eneo la Chuo cha Maendeleo ya Wananchi ( MWAMVA) kilichopo katika Halmashauri ya Mji wa Kahama Mkoani Shinyanga,vimegawiwa kwa wananchi kimakosa na
kusababisha mgogoro mkubwa baina ya chuo na  waliotwaa maeneo hayo.

Umilikishwaji huo wa Viwanja na kuibua msigano,ni muendelezo wa maeneo ya awazi ama yanayomilikiwa na taasisi za serikali na kidini yakiwemo makaburi,kupokwa na kufanywa vya makazi.

Akizungumza  na Wenyeviti wa Serikali za Mitaa na Vijiji juzi,katika Ukumbi wa Halmashauri ya Mji wa Kahama,Mkurugenzi Mtendaji wa Halamashauri hiyo,Anderson Msumba,alisema tatizo hilo limechangiwa na kutowajibika kwa weledi na watendaji wa Idara ya Ardhi ,watendaji wa kata pamoja na Wenyeviti wa Vijiji na Mitaa.

Msumaba alikiri ukosefu wa uwajibikaji unaozingatia maadili ya kazi na uliotawaliwa na maslahi binafsi imekuwa kiini cha migogoro ya Ardhi katika mji wa Kahama ambayo imekithiri  na kusababisha malalamiko mengi kutoka kwa wananchi.

Alisema kuwepo mkwa migogoro hiyo pia kumechangia kudumaa kiuchumi kwa jamii ambayo imekutwa ikigonganishwa katika kiwanja kimoja zaidi ya watu watatu,hivyo badala ya wananchi hao kufanya kazi kuinua vipato vyao ambavyo huwa sababu ya kuijenga Kahama,wamekuwa wakitumia muda wao mwingi kuhudhuria mahakamani na si kujenga Taifa.

Aidha aliwaeleza wenyeviti hao kuwa tayari  ofisi yake  kwa kushirikiana na baraza la Madiwani  ameunda  tume  kwa ajili ya kuchunguza migogoro hiyo na kwamba tayari  imekwisha anza kazi  sehemu mbalimbali za mji huo na kuwataka wenye viti kutoa ushirikiano kwa tume hiyo ili kutatua migogoro ya ardhi iliyopo.

Hata hivyo Msumba aliwataka wenye viti hao kutojishirikisha na suala la ugawaji wa Ardhi  ili kujiepusha na migogoro baina yao na wananchi nakuongeza kuwa waendele kuwaongozi wananchi katika mitaa yao kwa kufuata misingi na kanuni za nchi bila kuvunja sheria.

Alisema  kuwa mji wa Kahama umekuwa unakuwa kwa kasi kila kukicha  kutokana na ongezeko la wageni wengi ambao wamekuwa wakiingi kwenye mji huo kwa kutaka viwanja kwa ajili ya uwekezaji na makazi hivyo ni vyema wakaepuka kujiingiza kwenye hali hiyo.

Kwa upande wao wenye viti hao waliahidi kushirikiana kwa pamoja na Halmashauri katika shughuli mbalimbali za maendeleo ya wananchi ili Halmashauri ya mji wa Kahama iweze kusonga mbele.


KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI