Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania John Pombe Magufuli amesema Kampuni
ya madini ya Barrick imekuabali kufanya mazungumzo na Serikali ikiwa ni
pamoja na kulipa
fedha ambazo Serikali inadai kwa kufanya shughuli zake
hapa nchini.
Mazungumzo hayo yamekuja baada ya Serikali kudhibiti makontena 277,yaliyoundiwa Kamati mbili za Rais,ambazo zote ziliwasilisha taarifa ambazo zilizidisha msimamo wa Serikali kudhibiti mchanga huo kutosafirishwa baada ya kubaini kampuni ya Acacia kufanya kazi kinyume cha sheria kutokana na kutokuwa na Usajili;Brela,huku ikihujumu mapato yatokanayo na usafirishaji wa mchanga wa dhahabu ( Makinikia ).
Akizungumza mara baada ya kukutana na
kufanya mazungumzo na Mwenyekiti wa Kampuni ya Barrick Gold Corporation
inayomiliki kampuni ya Acacia Mining Limited Prof. John L. Thornton leo
Ikulu jijini Dar es Salaama, Rais Magufuli amesema kampuni ya Barrick
imekubali mazungumzo na Serikali ya Tanzania na kulipa fedha
wanazodaiwa.
“Serikali
inakaribisha mazungumzo hayo na itaunda jopo la wataalamu watakaofanya
majadiliano na kampuni ya Barrick Gold Corporation ilikufikia
makubaliano ya kulipwa fedha zinazodaiwa na kampuni hiyo itakavyoendesha
shughuli zake nchini maslahi ya pande zote mbili” alisema Rais
Magufuli.
Rais
Magufuli alisema kuwa licha ya kampuni hiyo kukubali kulipa fedha
wanazodaiwa Prof. John L. Thornton amekubali kushirikiana na Tanzania
kujenga mtambo wa kuchenjulia dhahabu hapa nchini.
Naye,
Prof. John L. Thornton amesema kampuni yake ipo tayari kufanya
mazungumzo na Serikali ya Tanzania yatakayozingatia maslahi ya pande
zote mbili ikiwa ni pamoja na kulipa fedha zote ambazo inatakiwa kulipa
kwa Serikali ya Tanzania.
Mazungumzo
hayo kati ya Rais Magufuli na Mwenyekiti wa Kampuni ya Barrick
yalihudhuriwa na Balozi wa Canada nchini Ian Myles na Waziri wa Katiba
na sheria Prof. Palamagamba Kabudi.
KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI