Tuesday, May 2, 2017

UHABA WA MAJI WAKOSESHA MASOMO WANAFUNZI

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO



TATIZO sugu la Maji linaloikabili Kata ya Mwanase katika Halmashauri ya Msalala,wilayani Kahama,limekuwa chanzo cha Wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya
Mwamandi,kusoma kwa saa moja,huku muda mwingi wakitumia kuchota maji.

Wanafunzi wa Shule ya Sekondari hiyo,iliyopo katika Kata ya Mwanase,kwa siku hutumia muda huo kusoma masomo,kutokana na muda mwingi kuutumia kwa ajili ya kupata maji ya kukidhi mahitaji ya shuleni,ambayo huyachota umbali mrefu.

Diwani wa Kata ya Mwanase ilipo Shule hiyo ya Sekondari,Samson Paul, alisema hayo juzi katika kikao cha Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Msalala,kwa kusema tatizo hilo linaathari katika sekta ya elimu,kutokana na wanafunzi kulazimika kutembea umbali wa kilometa mbili kwa ajili ya kupata maji kwa matumizi ya shule.

Alisema wanafunzi hao wanakwenda  shuleni kwa ajili ya kuhudhuria masomo yao ya kila siku,lakini Walimu wao huwaamuru kufanya kazi ya kusomba maji kutoka katika shule ya msingi  Mwanase ambayo ipo umbali wa kilometa mbili,kitendo ambacho husababisha kuhudhuria masomo kwa saa moja kutokana na foleni wanayoikuta kwenye bomba.

Diwani huyo aliendelea kusema kuwa mbali na tatizo la maji liliopo katika shule hiyo, pia Shule hiyo inakabiliwa na upungufu mkubwa wa walimu kwani kuna Walimu watatu tena wa kiume tu,wanaolazimika kufundisha zaidi ya Wanafunzi 600 katika sekondari hiyo.

Aidha alisema kuwa kutokana na upungufu huo wa walimu katika Sekondari hiyo kumepunguza hali ya ufaulu kwa kiasi kikubwa na kuitaka Halmashauri hiyo kuangalia  suala hilo kwani hata kwa mwaka huu kunaweza kukawa na ufaulu mdogo wa Wananfunzi katika sekondari hiyo

“ …tunaomba tutatuliwe shida ya maji iliopo katika kata yetu hasa kwa Wanafunzi wa shule ya sekondari ya Mwamandi ambao wanakosa Masomo yao kwa muda muafaka,kwani muda mwingi wanapoteza vipindi vyao katika kusomba maji kwa ajili ya matumizi shule”, alisema Paul.

Hata hivyo Diwani huyo alisema kutokana na tatizo hilo la maji katika kata hiyo pia kumesababisha Walimu wanaopangwa kufundisha katika shule hiyo kukimbia huku wachache waliopo kufanya maamuzi magumu ya kuishi mjini, hali ambayo inachochea ufaulu mdogo kwa Wanafunzi wa shule hiyo kila mwaka .

Hata hivyo Mhandisi wa Maji katika Halmashauri hiyo,Cyprian Ndabavunye alisema kuwa  Halmashauri imepanga kupeleka maji katika Kata hiyo katika mwaka ujao wa fedha kutokana na kutokuwemo katika bajeti ya mwaka 2017/2018.

Amebainisha sababu ni kutokana na mwaka huu viongozi wa Kata hiyo walichelewa kuwasilisha bajeti yao kwaajili ya kuingizwa kwenye orodha ya miradi itakayotekelezwa na kuwasihi wananchi wa Kata hiyo kuwa wavumilivu katika kipindi hiki.

KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI