Wednesday, May 3, 2017

HALMASHAURI KAHAMA ZAANZA KUTEKETEZA FISI

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO



KUFUATIA matukio ya wanyama aina ya Fisi kutishia usalama wa wananchi hususani watoto wadogo wanaoenda shuleni nyakati za asubuhi katika vijiji,Wilayani Kahama,Kamati ya
Ulinzi na Usalama wilayani humo imeamua kudhibiti hali hiyo.

Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya,imetoa maelekezo kwa Halmashauri za Msalala na Ushetu sambamba na Mji wa Kahama,kuanza zoezi la kuteketeza wanyama hao,ambao wamekuwa wakiingia katika makazi ya watu kufanya usumbufu wa kushambulia mifugo pia binadamu.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Msalala,Simon Berege,ametoa taarifa juu ya kuanza zoezi hilo wakati akizungumza na wandishi wa Habari hivi karibuni ofisini kwake  baada ya kikao cha kawaida cha baraza la Madiwani wa Halmashauri hiyo ambacho kililenga kujadili mambo mbalimba mbali ya maendeleo.

Berege aliwambia wandishi wa Habari kuwa kwa sasa halmashauri hizo mbili, Msalala na Ushetu zinaendesha zoezi la kuwasaka fisi hao wanaotishia maisha ya wananchi na kuwaua kwa kutumia bunduki ili kunusuru maisha ya wananchi hao.

“Hawa fisi wakiingia vijijini wanatishia maisha ya wananchi hasa wanawake na watoto, lakini fisi hawa wanawaogopa wanaume hivyo kwa ruhusa ya kamati ya ulinzi na usalama ya Wilaya tumeanzisha oparesheni maalumu ya kuwatokomeza fisi kwa kuwaua kwa kutumia bunduki na sumu,” Alisema Berege.

Alisema inashangaza kwa wanyama hao kushambulia watoto na wananwake huku wakionesha kuwaogopa wanaume,hivyo kuwataka wananchi kutoa ushirikiano juu ya zoezi hilo na kuwahi kutoa taarifa pindi inapotokea hali ya hatari juu ya fisi wanaozagaa katika maeneo yao  ili iwe njia rahisi ya kupambana nao.

Aliongeza kuwa siku hiyo wakati akizungumza na wandishi wa Habari ofisini kwake tayari fisi mmoja aliuawa na watu wa idara ya wanayama pori katika Kata ya chela baada ya kutaka kutafuna watoto na kutaja idadi ya jumla ya fisi waliouwawa kuwa ni fisi 14.

Akifafanua zaidi juu ya idadi ya fisi waliouawa ili kuwanusuru zaidi wananchi kuliwa na fisi hao Mkurugenzi huyo alisema kuwa  katika kikijiji cha Kakola waliuawa fisi 7 Kata ya Ngaya waliuawa fisi 6 na Kata ya Chela aliuawa fisi mmoja (1) kulingana na vijiji hivyo kuwa na mabonde pamoja na mapango mengi zoezi hilo litakuwa endelevu.

KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI