Saturday, April 8, 2017

WATAKIWA KUMILIKI MITUNGI YA ZIMA MOTO KWENYE NYUMBA ZA MAKAZI.

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO



JESHI la Zimamoto na Uokoaji wilaya ya Kahama,mkoani Shinyanga,limewataka wakazi wa mji wa Kahama,kukabiliana na majanga ya moto kwa kumiliki
vifaa vya kudhibiti dharura hizo majumbani mwao.

Limesema jamii pindi ikijenga utamaduni wa kuweka mitungi ya zima moto kwenye nyumba  za makazi yao sambamba na  sehemu za biashara zao itajinusuru na  ajari za moto zinazoweza kujitokeza,na kuwasbabishia hasara za kiuchumi,anaandika Shaban Njia.

Mkuu wa Kitengo cha Jeshi la zima moto na uokoaji wilayani Kahama,Mkaguzi Msaidizi Frank Elophazy,ametoa ushauri huo kwa kubainisha kwamba kuwepo kwa mitungi hiyo katika maeneo hayo, kutasaidia kudhibiti kwa haraka viashiria vya majanga ya moto.


Meshack anasema pindi majanga ya moto yanapojitokeza huathiri kichumi kwa kijamii inayokumbwa na kadhia hiyo,inayotokana na uzembe wa kushindwa kuchukua  hadhari kwa kuweka mitungi ya zima moto katika nyumba zao ama sehemu mbali mbali za biashara.

Anasema;“Wanakahama wanatakiwa kujenga desturi ya kuweka mitungi ya zima moto katika nyumba zao,hatua itakayosaidia kupunguza wimbi la moto,kwa kujihudumia hatua za awali kabla ya jeshi la zima moto kufika katika eneo la tukio.”


Anabainisha kazi ya jeshi hilo  ni kufanya ukaguzi wa kina  na uokozi pindi yanapotokea majanga ya moto,huku akiikumbusha jamii kutakiwa kujenga nyumba zao kwa kufuata ramani na sheria pia kanuni za miji,kwa kuweka miundo mbinu rafiki ya uokozi iwapo itajitokeza janga la moto.

“Tumeweza kutoa elimu sehemu mbalimbali juu ya matumizi ya mitungi ya zima moto katika jamii hususani mashuleni, kwenye masoko na majumbani pamoja na sehemu za biashara,kuweza kupunguza tatizo la ajali za moto zinapotokea,ikiwa ni pamoja na kuokoa mali zao,” anasema Meshack.

Aidha anawasisitiza wananchi kununua kwa wingi mitungi hiyo ya zima moto ili kuepukana na ajali za moto zisizokuwa za lazima na kuongeza kuwa kipindi inatokea ajali ya moto wakumbuke kupiga simu mapema ili kuokoa mali zao.

Hata hivyo anabainisha kwamba nyumba nyingi katika wilaya ya Kahama zimejengwa bila kufuata utaratibu wa mipango miji na kanuni zake za ujenzi hali amabayo inasababisha mali nyingi kuteketea na moto kutokana na gari za zima moto kushindwa kuwafikia kirahisi ili kutoa huduma hiyo ya zima moto,pindi janga la moto linapotokea.

“Tuwaombe wananchi pindi wanapotaka kuanzisha ujenzi wa nyumba za kuishi na biashara wakitoka idara ya ardhi waweze kufika ofisi zetu kusudi tuwape ushauri namna nyumba zao zijengwe ili kuwezesha timu ya uokozi kutoka jeshi la zima moto kufika kirahisi na kuokoa mali,pindi wanapokabiliwa na janga la milipuko ya moto,” anahitimisha Meshack.





KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI