Saturday, April 8, 2017

SERIKALI YASHTUSHWA KUTEKWA KWA ROMA MKATOLIKI.

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO



SERIKALI imedai kupokea kwa mshtuko,taarifa za kutoweka kwa Mwanamuziki,Ibrahim Mussa,almaarufu kwa jina la Kisanii;“ Roma Mkatoliki.”

Katika taarifa yake,kupitia Wizara ya Habari, Utamaduni, sanaa na Michezo imesema imepokea kwa mshtuko taarifa za kutoweka kwa msanii huyo tangu tarehe 5 Aprili 2017, na kuomba wananchi washirikiane na vyombo vya Dola,kuhakikisha anapatikana.

Taarifa hiyo ya Serikali,ilitolewa  jana jioni na kusainiwa na Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini wa wizara Zawadi Msall,imeeleza Wizara hiyo ambayo ndiyo inadhamana na tasnia ya sanaa,imefuatilia kwa kina suala.

Imedai kwa kuwa tukio hilo lina muelekeo wa jinai na kwamba kwa mujibu wa taarifa kutoka vyombo vya dola vilivyothibitisha kutomshikilia katika kituo chochote cha Polisi,ni vyema jitihada zikafanyika za kupatikana sambamba na wenzake.

Hivyo Serikali imewaomba wadau mbalimbali na wananchi kwa ujumla kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi kwa kutoa taarifa zozote zitakazo saidia kujua alipo msanii huyo.

Roma Mkatoliki akiwa na wasanii wenzake wawili,imedaiwa kutekwa wakiwa katika shughuli zao za kawaida za kisanii katika studio,ambapo watekaji hao waliondoka na baadhi ya vifaa vya studio.

Hili ni tukio la pili kubwa nchini kutokea,baada ya hapo awali msaidizi wa masuala ya Kisiasa wa Mwenyekiti wa Taifa wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo “CHADEMA”,Freeman Mbowe;aitwaye Ben Sanane,kutoweka hadi leo hajulikani alipo.

KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI