Saturday, April 8, 2017

RC MWANZA AKEMEA MAAFISA UVUVI

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO



MKUU  wa Mkoa wa Mwanza,John Mongella, amejitokeza na kudai vitendo vya uvuvi haramu vinavyoendelea vinabarikiwa na baadhi ya baadhi ya Maafisa kwa
maslahi yao binafsi.

Uwepo wa Maafisa uvuvi hao wasio waaminifu,wasiozingatia weledi wa majukumu yao,kutokana na kushirikiana na wavuvi haramu,ni janga linaloiangamiza Taifa,anaandika Tunu Herman.

Mkuu huyo wa Mkoa anasema kitendo cha Wavuvi  kuendelea kuvua samaki kwa njia haramu kunachangiwa na Maafisa Uvuvi,ambao huwakamata kisha huwaachia pasipo kuwachukulia hatua kali za kisheria zenye maslahi ya Taifa.

Amesema vitendo vya kuwakamata kisha kuwaachia bila sababu maalumu,linaipotezea Serikali Rasilimali nyingi zinazotumika kupambana na tatizo hilo,ambazo zingeelekezewa katika kutatua changamoto zinazo ikabili jamii.

Akiwa katika  eneo la Mwalo wa Kirumba,kufuatia  tukio la kukamatwa kwa samaki kilogram 3482 wenye thamani ya Shilingi Milioni 20,892,000/= waliovuliwa kinyume cha sheria na kusafirishwa kwa njia ya magendo,anasema, vita hivyo haviwezi kufanikiwa ikiwa Maafisa uvuvi wataamua kuendelea kushirikiana na Wavuvi hao haramu.

Anasema,"Kama Maafisa wa Serikali, wakiwa ndio vinara wakuwasaidia wavuvi haramu ni bora tukafanye kazi zingine, maana kama mtu  anakamatwa na kuachiwa kwa  ujanjaujanja kwa  ajili ya Masilahi binafsi ambayo yanaleta madhara kwa  wananchi na serikali kwa  ujumla, hakuna haja ya kuwekeza nguvu kubwa katika mapambano hayo.”

“…haiwezekani kupambana   kutokomeza Uvuvi haramu kuwe tatizo kwa Serikali,kumbe  kuna watu wananufaika,hawana uchungu na  maslahi ya Taifa,kwani wameendekeza tamaa,pasipo kujali wanalipwa mshahara na serikali,inayotokana na kodi za wananchi," alisema Mongella.

Aidha Mongella alimuagiza Mkuu wa Kituo cha Polisi Kirumba,Susan Kidiku na Kamanda wa Takukuru mkoani Mwanza, Ernest Makale,kumkamata na kumfanyia uchunguzi Ofisa wa Uvuvi wa wilaya ya Ilemela,Ivon Maha,aliyehusika kumkamata na kumuachia Mfanyabiashara aliyekamatwa na samaki zaidi ya tani tano.

Mfanyabiashara huyo,Mageta Bigamboa,alikamatwa akitokea wilayani  Ukerewe,akiwa na samaki zilizobebwa kwenye gari aina ya Mistubishi Fuso lenye namba T 202 BGE ambalo ni mali ya Magireti Agustino.

Ameagiza hatua za kisheria zichukuliwe kwa wakati,kutokana na mtumishi huyo wa serikali,kuchambua kisha kuruhusu tani mbili za samaki kuondoka bila  kibali cha  chakusafirishia,huku akitambua mhusika aliyemuidhinisha hakuwa na Leseni ya biashara.

Agizo hilo lilitolewa na Mongella, kufuatia maelezo yakubabaisha yaliyotolewa na Afisa Uvuvi huyo kudai, kufuatia kukamatwa kwa Samaki hao  na Taasisi ya kupambana na rushwa  wao kama wataalam wa masuala ya samaki waliwachambua,kisha kubaini kilo 2,316 wenye thamani ya Shilingi 13,896,000/- kukidhi viwango.

Afisa Uvuvi  huyo anajitetea kwa kudai maamuzi hayo kuyatoa kushirikiana na Maafisa wa TAKUKURU,kuruhusu samaki hao wachukuliwe na mhusika,jambo ambalo linakanushwa vikali na Mkuu wa Takukuru mkoani Mwanza,mbele ya Mkuu wa mkoa huyo.

"Mkuu wa Mkoa, sio kweli kwamba TAKUKURU, tullishiriki kuwaachia samaki hao walio chambuliwa, kwani sisi mara baada ya kuwatia mbaroni wahusika, tulichokifanya nikuwaita waatalaam wavuvi na kuwakabidhi samaki lakini tukaondoka na kibali husika kilichokuwa kinatumika kuwasafirishia samaki hao," alisema Mkuu wa Takukuru Mkoani Mwanza,Makale.

Mkoa wa Mwanza upo katika Mapambano ya vita dhidi ya Uvuvi haramu,tayari Nyavu za makila na Zana zingine za uvuvi haramu zimeisha kamatwa kwenye maeneo ya Buchosa, Ilemela, Sengerema  na Ukerewe na  kuteketezwa kwa Nyakati tofauti

Kwa mujibu wa Sheria ya Uvuvi namba 22 ya Mwaka 2003 na kanuni zake za Mwaka 2009 ni makosa kuvua samaki aina ya  Sangara waliochini ya Sentimita 50 ambao wanatajwa kama samaki wachanga, pia inakataza kuvua samaki walio zaidi ya Sentimita 85, ambao huuchwa kwaajili ya mazalia ya Samaki.

KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI