Saturday, March 18, 2017

YANGA YAPATA SARE NA KUANGUKIA KOMBE LA SHIRIKISHO.

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO



MABINGWA watetezi wa Ligi Kuu Tanzania bara,Yanga African ya Jijini Dar Es Salaam,imeangukia katika michuano ya Kombe la
Shirikisho,baada ya kushindwa kuingia hatua ya robo fainali ya Michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika.

Yanga imeshindwa kufuzu hatua hiyo baada ya kutoshana nguvu na timu ya Zanaco ya Zambia,ambayo imefuzu hatua hiyo kwa faida ya bao la ugenini.

Katika mechi ya kwanza, Yanga ililazimishwa sare ya mabao 1-1kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam,hivyo kutakiwa ili imudu kufuzu ni budi kutoka sare ya mabao 2-2 na kuendelea. Au ushindi wa aina yoyote.Jambo ambalo wameshindwa kulifanya katika uwanja wa Taifa wa Mashujaa mjini Lusaka,Zambia.

Katika pambano hilo hadi timu zinakwenda mapumziko zilikuwa zimetoshana nguvu,pamoja na timu hizo kushambuliana kwa zamu,lakini safu za Ulinzi kwa kila upande ulikuwa makini na kusababisha mpira kuchezwa kati zaidi.

Dakika ya  45 mchezo,Haji Mwinyi,alitaka kuigharimu timu yake ya Yanga baada ya kufanya uzembe kwa kutoa pasi fupi,na kusababisha Mlinda Mlango wake,Deogratias Munis “Dida”kufanya kazi ya ziada kuokoa hatari hiyo.

Katika pambano hilo,Mwamuzi kutoka nchini Kenya,aliwazawadia Kadi ya Njano wachezaji wa Yanga;Kelvin Yondani mnamo dakika ya 37 ya mchezo,baada ya kumuangusha Sikala na Haji Mwinyi mnamo dakika ya 75,kwa kumuangusha Musonda.


 
 






KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI