TIMU
ya Soka ya Kabela City ya wilaya ya Kahama,Mkoani Shinyanga,imefanikiwa kusonga
mbele katika Michuano ya Kombe ya Shirikisho la Soka Nchini"TFF",baada ya
kuisambaratisha timu ya
Murusagamba FC kutoka Mkoa wa Kagera,kwa kipigo cha bao 4 – 0.
Murusagamba FC kutoka Mkoa wa Kagera,kwa kipigo cha bao 4 – 0.
Ikicheza
mbele ya umati wa mashabiki wake waliofurika katika uwanja wa Halmashauri ya
Mji wa Kahama,Kabela City ilitandaz soka safi na kuonesha dhamira ya kufika
mbali kwenye michuano ya kombe la FA maarufu kama kombe la Azam;anaripoti
Paschal Malulu.
Timu
ya Murusagamba FC ililianza pambano hilo kwa kasi,ambapo walifanya mashambulizi
kwenye lango la Kabela City hali hiyo
iliwapa wakati mgumu mashabiki wa timu mwenyeji kuwa na matumaini ya kuibuka na
ushindi.
Hata
hivyo Murusagamba FC pamoja na kulisakama goli la Kabela City kwa dakika tisa
mfululizo hawakufanikiwa kupata bao,mnamo dakika ya kumi ya mchezo vijana wa Kabela
City waliamka na kuanza kujibu mashambulizi kwa kulisakama lango la wapinzani wao.
Vijana
wa Kabela City walifanikiwa kupata bao la kuongoza mnamo dakika ya 12 ya mchezo
lililofungwa kwa kichwa na Elias Kisusi baada ya kupokea kona maridadi
iliyopigwa na Abuu Wakati.
Mnamo Dakika
ya 15 Murusagamba FC walipata penati tasa baada ya mchezaji wake kupiga shuti
kali na mpira huo nje ya lango.
Katika
dakika ya 19 mchezaji Mkiwa Bonzo aliwanyanyua mashabiki wa Kabela City kwa
kuandika bao la pili na kuendelea kuwapa wakati mgumu wapinzani wao kusawazisha
mabao hayo, hadi mapumziko bao zilikuwa 2 -0.
Kipindi
cha pili kilinza kwa timu zote kushambuliana kwa kutengeneza nafasi za kupata
bao dakika ya 52 Mkiwa Bonzo akarejea kambani kwa kufunga bao la tatu kwa timu
ya Kabela City,kabla ya dakika ya 76,Mkiwa Bonzo tena kupachika bao la nne,na
kufanikiwa kupiga tatu za kwake (hat-trick).
Baada
ya pambano hilo,Kocha wa timu ya Kabela City,Joshua Maganga alisema ni kazi
nzuri vijana wake wamefanya,na wanastahili ushindi kwa kuwa wanacheza kulingana
na maelekezo anayowapatia na na kusisitiza wataendelea namazoezi makali ambayo
yatawasaidia kufanya vyema katika kombe hilo.
“…sisi
kila mechi ni fainali na timu iwe ya wapi hapa nyumbani kutufunga sio rahisi
sisi kila anaekuja usoni kichapo tangu ligi ya wilaya hatujawahi kufungwa sisi
kufungwa kwetu ni sare mashabiki waendelee kutushangilia tu”.Alisema
Maganga.
Kwa
upande wake nahodha wa Murusagamba FC,Ibrahimu George alisema kuwa moja ya
sababu ya kufungwa kwao ni maamuzi ya mwamuzi wa mchezo huo ambapo alikuwa
anatoa lugha ambazo zilichangia kuwatoa mchezoni wachezaji wa timu hiyo.
“ilikuwa
mwamuzi nikimfuata kuhusu maamuzi anayotoa anatoa lugha za matusi kweli ilikuwa
ni ngumu kwetu kushinda lakini niseme tumekubali matokeo”.Alisema.
Timu
ya Kabela city sasa ina subiri ratiba ya mshindi wa mchezo kati ya Jangwani ya
mkoani Rukwa dhidi ya Bagamoyo FC ya mkoani Pwani ambapo mchezo huo unataraji
kupigwa January 15 ama 16 kwa Kabela City kusafiri kwenda mkoani Pwani ama
mkoani Rukwa.
MWISHO.
KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI