Thursday, December 8, 2016

POLISI SHINYANGA KUSAKA MAJAMBAZI SUGU

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO






KATIKA kukomesha uharifu na kuhakikisha sherehe za Krisimasi na Mwaka Mpya zinasherehekewa kwa amani,Jeshi la polisi mkoani Shinyanga limeanzisha opresheni maalumu kwa  kutumia vitabu vya kumbukumbu za zamani kusaka majambazi sugu na kufanikiwa kukamata wanane.
 
Mkakati wa Opresheni hiyo umeanzishwa baada ya vitendo vya kiharifu wa kutumia silaha kuanza kujitokeza kwa kasi tangu mwezi Oktoba mwaka huu,na kuanza kuwatia hofu wakazi wa mkoa wa Shinyanga.
 
Akiongea na Waandishi wa habari mjini Kahama,Kamanda wa Polisi mkoa wa Shinyanga, Murilo Jumanne,alisema   katika uchunguzi wa awali wa Jeshi hilo ulibaini matukio hayo kuibuka baada ya waharifu waliokuwa wamefungwa na baadae kuachiwa kwa kukata rufaa na wengine kumaliza adhabu zao.
 
Kamanda Jumanne alifafanua kuwa kwa mujibu wa sheria za nchi,kukata rufaa kwa mhalifu ni haki yake,lakini kitendo hicho hakiwakatishi tamaa bali watawajibika kwa kufuata kanuni za jeshi la Polisi kuzuia uhalifu kwa kuwasaka wote ambao vitabu vyao vya kumbukumbu vinaonesha ni waharifu na majambazi sugu wa kutumia silaha.
 
Alisema tangu mwezi Oktoba mwaka huu,uharifu ulianza kujitokeza kwa kasi katika wilaya za Kahama,Shinyanga na Kishapu,hivyo kurejea katika vitabu vyao vya kumbukumbu za waharifu kubaini wapo wapi ndipo walipobaini   wengi wameachiwa kwa rufaa na wengine kumaliza vifungo vyao.
 
“Tulipobaini kuwepo kwa waharifu nje,tulijiuliza kwanini vitendo hivyo vianze wakati watu hao wakiwa uraiani?” Alihoji Kamanda Jumanne.
 
Kufuatia hali hiyo upelelezi ulianza kuwafuatilia  na kubaini kundi moja la majambazi wanane wakiwemo wanawake wanne ambao wamekamatwa wakiwa na bunduki 2 shoti gun ambazo zimekatwa mtutu na kuonekana kama bastola.
 
Pia kamanda Jumanne alisema watuhumiwa hao walikutwa na pikipiki 2 zenye namba moja   MC476 BHA ambazo zimedaiwa kutumiwa kuwapeleka kwenye matukio ya uharifu na kuongeza kuwa katika upelelezi huo mtuhumiwa mmoja Amosi James au maarufu kwa jina la George alifariki baada ya kupigwa risasi na polisi.
 
Katika tukio hilo mtuhumiwa huyo alikamatwa na bunduki 3 moja SMG na mbili shoti gun na risasi 38, risasi 30 zilikuwa kwenye magazine na aliwashawishi polisi ana bunduki nyingine kwa mganga wa jadi maeneo ya Busoka na baada ya kufika huko aliruka kwenye gari na kuanza kukimbia hali iliyofanya kupigwa risasi na baadaye kufariki wakati anapelekwa hospitalini.
 
Kamanda Jumanne,alisema  baada ya kufanya upelelezi juu ya mtuhumiwa huyo na kundi lake walibainika kufanya uharifu katika maeneo mbalimbali ya kanda ya ziwa ikiwemo Kahama, Shinyanga, Bukombe, Mbogwe na Geita na alikuwa amefungwa gerezani na akatoka kwa rufaa.
 

KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI