IMEFAHAMIKA
vitendo vya unyanyasaji wa kingono kwa watoto wa kike wanaosoma Shule za
Sekondari wilayani Kahama vimekithiri na kusababisha wanafunzi 21 wa Shule za
Sekondari za Kata katika
Halmashauri ya Mji wa Kahama,kukatisha masomo kutokana
na kupata ujauzito.
Katika
utafiti uliofanywana Shirika lisilo la Kiserikali la SHDEPHA+ la wilayani
Kahama,limebainisha takwimu za wasichana hao kukatisha masomo kwa kupewa
ujauzito ni kuanzia mwezi Januari hadi
kuishia mwezi Septemba mwaka huu.
MKURUGENZI Miradi SHDEPHA+,Venance Mzuka akiongea. |
“…walichofanyiwa
ni unyanyasaji wa kijinsia,na vitendo hivyo vikifumbiwa macho ni hatari kweli kwa
taifa kutokana na wasichana hao kukatishwa masomo yao,”alisema Mzuka.
WANAHABARI wakisikiliza kwa makini |
MZUKA akikisisitiza jambo kwa Wanahabari |
WAANDISHI wa Habari;Shija Felician na Pili Jitoba. |
“….wabakaji
hao hufanya maelewano,kisha kulipa fedha au mifugo,na familia wa binti na kesi
hizo kuzimalizia majumbani,huku wazazi ama walezi wakiandaa hadaa ya kutotiwa
hatiani,”alisema Barnabas.
MZUKA akifafanua jambo kwa Waandishi wa Habari |
Mkurugenzi
wa Halmashauri ya mji wa Kahama,Anderson Msumba,alikiri kuripotiwa kwa baadhi
ya wanafunzi kukatiza masomo kutokana na mimba,kiasi cha kuamua kukabiliana na
hali hiyo kwa kuweka utaratibu wa kupima mimba kwa wanafunzi wa kike kila baada
ya miezi mitatu.
KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI