Thursday, October 20, 2016

ACACIA YAKABILI MIGOGORO KWA KUCHANGIA MAENDELEO.

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO



MGODI wa dhahabu wa Bulyanhulu,unaomilikiwa na Kampuni ya Acacia,umetakiwa kudumisha mahusiano na majirani wanaozunguka uwekezaji wake,na kuhakikisha unakuwa mstari wa mbele kuchangia miradi
inayoibuliwa na wananchi.

Aidha umetakiwa kubaini na kuondoa kero zinazowakabili wananchi wa wanaoishi kumzunguka mwekezaji huyo,hatua itakayozidi kuchangia kuwepo kwa maendeleo ya miradi ya wananchi,itakayokuza uchumi,na kuondokana na migogoro kama inayotokea maeneo mengine ya wawekezaji nchini.

Mkuu wa Wilaya ya Nyang’wale mkoani Geita, Hamimu Gwiyama,anapongeza mahusiano mazuri yaliyopo baina ya Mgodi wa Bulyanhulu na vijiji vinavyouzunguka.

Anasema ameridhishwa na mahusiano makubwa aliyoyakuta kwenye Wilaya jirani ya Kahama Mkoani Shinyanga na wawekezaji wa mgodi wa Bulyanhulu kwa madai yamechangia kuwepo kwa maendeleo,katika eneo husika.

Akiongea kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Kahama Fadhil Nkurlu,katika uwanja wa shule ya msingi Kakola Kata ya Bulyanhulu Halmashauri ya Msalala wilayani Kahama,Gwayima aliupongeza mgodi kwa kudumisha mahusiano ambayo yamekuwa chachu ya maendeleo kwa wananchi.

Alisema kuna maeneo nchini kuna migogoro baina ya wawekezaji na wananchi,na kudai wakati umefika kwa wawekezaji na wananchi kwa pamoja kuwa na mahusianao mazuri ili kuweza kuwa na uwekezaji wenye tija kwa pande zote mbili kwa kuharakisha maendeleo ya nchi.

“Mashirikiano  haya mazuri naomba myadumishe kwani Mgodi utapokuwa na mahusiano mazuri na wananchi wanaozunguka maeneo yake, kutasaidia utekelezaji mzuri wa miradi mbalimbali ya maendeleo kwa wakazi,wanaoishi katika vijiji  14 vinavyozunguka mgodi.”Alisema Mkuu huyo wa wilaya.

Aidha Gwiyama alisema pasipo mahusiano mazuri mgodi hautaweza kutekeleza shughuli za maendeleo kwa wakazi hao,  ambao ni jirani zao, badala yake itatawala migongano isiyokuwa na tija baina ya wakazi hao na uongozi wa mgodi.

“Ni wapongeze kwa kitendo cha uongozi wa Acacia kubuni mbinu ya kunyanyua vipaji vya michezo mbalimbali sehemu anayowekeza ni jambo jema,hali hii inaonyesha wazi wanania ya dhati ya kuwasogeza karibu Wananchi waliopo sehemu wanayowekeza” alisema  Gwiyama.

Aliongeza kwa kusema,“Niwaase uongozi wa mgodi huu,msiishie kudhamini leo tu,tafadhari endeleeni kufadhili michezo mbalimbali kwa Wananchi wa halmashauri ya Msalala na ibueni vipaji hivyo ili tupate wachezaji wa kimataifa kutoka Msalala na pia mshirikishe na washiriki kutoka Wilaya yangu ya Nyang’hwale  

Kwa upande wake Meneja  Mahusiano ya jamii wa Acacia Bulyanhulu, Sara Terry, alisema  lengo la Mgodi ni kudumisha mahusiano baina ya Wananchi na mgodi huo,ndio sababu ya kufadhili bonanza hilo,hali itakayodumusha amani na kuufanya mgodi kutekeleza shughuli za maendeleo kwa wananchi pamoja na kufanya shughuli za uwekezaji ziwe za ufanisi zaidi.

Bonanza hilo liliandaliwa na shirika lisilo la kiserikali la Search for Common Ground linalofanya shughuli zake ndani ya mgodi wa Bulyanhulu ambapo hilo limefadhiliwa na kampuni ya Acacia ambapo mratibu wa Thomas Magesa alisema lengo lake ni kuimalisha mahusiano kutokana na shirika lake kujihusisha na maswala ya usuluhisho wa migogoro.

KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI