Monday, May 9, 2016

WAASWA KUJIUNGA VIKUNDI VYA UJASIRIAMALI ILI KUPATA MILIONI 50 ZA MAGUFULI

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO



WATANZANIA waishio vijijini wametakiwa kujiunga kwenye vikundi vya ujasiriamali ili wapate Sh.Milioni 50 za miradi ya maendeleo katika kila Kijiji zitakazotolewa na Serikali.

Ushauri huo umetolewa na Afisa Maendeleo ya Kata ya Isaka,Grace Nyahonge, katika Mkutano wa Hadhara  kwa kuwahadharisha kutopata fedha hizo zinazotokana na ahadi ya Rais John Magufuli,iwapo hawatakidhi vigezo.

Nae Diwani wa Kata hiyo,Dk.Gerald Mwanzia,amewaasa kabla ya kupata mikopo hiyo ni vyema wakajikita katika shughuli za ujasiriamali,na kutumia fedha hizo kuendeleza mitaji yao ili kupata ufanisi wa biashara zao.

Aidha Dk.Mwanzia ameiomba jamii izingatie kanuni za afya katika kuboresha afya zao na kuwa makini na kuhakikisha wanatunza mazingira wanayoishi vyema kusudi kuepuka uwezekano wa kupata magonjwa ya milipuko.

KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI