Tuesday, May 10, 2016

ACACIA KUONDOA TATIZO LA KUJIFUNGULIA KWA WAKUNGA.

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO



MGODI wa Dhahabu wa Bulyanhulu,unaomilikiwa na Kampuni ya Acacia,huenda ukasaidia kwa kiwango kikubwa tatizo la kujifungua wajawazito kwa Wakunga wa Jadi,kutokana na ufadhili uliotoa wa Shilingi Milioni 440 kwa Taasisi ya Benjamin Mkapa,ili kuboresha huduma ya Afya ya mama na mtoto.

Aidha imefahamika katika Halmashauri ya wilaya ya Msalala,asilimia 46 ya akina mama wajawazito,hujifungulia nyumbani wakihudumiwa na  wakunga wa jadi,kutokana na halmashauri hiyo kutokuwa na hospitali ya wilaya,hivyo kuwa sababu ya kutokea vifo vya akina mama hao na watoto wanaojifungua.

Mganga Mkuu wa Hospitali ya Halmashauri ya Msalala,Dk.Hamadi Nyembea,anabainisha hali hiyo wakati wa utiaji saini makubaliano ya TSH 440 Milioni baina ya Taasisi ya Benjamin Mkapa(BMF)na Mgodi wa dhahabu wa Bulyanhulu, kwa ajili ya mradi wa kuboresha huduma za afya ya uzazi wa  mama na mtoto.

MKURUGENZI Mtendaji wa BMF,Dk.Ellen Senkoro,Meneja Mgodi wa Dhahabu wa Bulyanhulu,Graham Crew(walioketi)Mkuu wa Wilaya ya Kahama,Vita Kawawa aliyesimama kulia(mwenye suti)pamoja na viongozi wa Halmashauri ya wilaya ya Msalala,BMF na Mgodi wa dhahabu wa Bulyanhulu,wakiwa na nyuso za furaha baada ya uwekaji wa saini wa Mkataba baina ya BMF na Mgodi wa Bulyanhulu.
Mgodi wa Dhahabu wa Bulyanhulu unaomilikiwa na Kampuni ya Acacia,umetia saini hati hiyo ya makubaliano baina yake na BMF,kutekeleza mradi huo kwa miaka miwili,ambapo,Dk.Nyembea alifahamisha hatua itakayosaidia kupata vituo bora vya afya katika Halmashauri ya Msalala,na kusaidia kupunguza vifo vya mama na mtoto.

“Halmashauri ya wilaya ya Msalala,hatuna hospitali isipokuwa na tuna vituo vichache vya Afya ambavyo vipo mbali na jamii kutokana na miundo mbinu ilivyo,na kulazimika kujifungulia kwa wakunga,na kusababisha kutokea kwa vifo,kuwepo mradi huu utasaidia kuboresha vituo vya afya ambavyo vitatoa huduma ya upasuaji wa dharura na kusaidia kupunguza vifo hivyo,”alisema Dk.Nyembea.

Kwa upande wake Mkuu wa wilaya ya Kahama,Vita Kawawa,alisema ufadhili huo wa Mgodi wa Bulyanhulu kwa Taasisi ya Benjamin Mkapa,utasaidia kwa kiwango kikubwa kuboresha huduma ya afya,kwa taasisi hiyo kutoa huduma ya afya moja kwa moja kwa wananchi walio pembezoni katika Halmashauri ya Msalala,kwa kuwaboreshea miundo mbinu na kusomesha wataalamu.  

Nae Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Benjamin Mkapa,Dk.Ellen Mkondya Senkoro,alisema taasisi yake inafanya kazi na serikali,ikiwa na lengo kubwa la kusaidia mkakati wa serikali,ambapo kupitia mradi huo wanatarajia kusaidia suala la miundo mbinu na wataalamu katika zahanati ya Kakola na Kituo cha Afya Cha Bugarama,ili kupunguza vifo vya mama na mtoto.

Meneja Mgodi wa Bulyanhulu,Graham Crew,alisema mgodi wake kupitia Mfuko wa Maendeleo umekuwa ukitoa ufadhili mbalimbali wa shughuli za Kijamii katika eneo linalozunguka mgodi huo na kupitia ufadhili walitoa utasaidia mapambano ya Ukimwi na kuboresha afya ya mama na mtoto,ambao ana imani mradi huo utatekelezwa kwa ufasaha na Mfuko huo wa Benjamin Mkapa.
MENEJA Mgodi wa dhahabu Bulyanhulu,Graham Crew na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Benjamini Mkapa,Dk.Ellen Senkoro,wakisaini Mkataba.

Akizungumzia Ufadhili huo,Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Msalala,Patrck Kalangwa,alisema pindi mradi huo utanufaisha wananchi zaidi ya 321,852 katika Halmashauri ya Msalala,kutokana na kusaidia kuondoa changamoto zinazokabili kwa kipindi hiki,ikiwemo nusu ya wajawazito kujifungulia nyumbani na kutopatikana huduma ya upasuaji wa dharura.

KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI