Monday, May 9, 2016

RAIS MAGUFULI ATETEA UTUMBUAJI MAJIPU

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO



RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,John Pombe Magufuli,ametumia fursa ya kuhudhuria ibada ya Jumapili,kwa kutetea maamuzi yake ya kuwatimua baadhi ya watumishi wa umma,wanaokiuka maadili,kwa lengo la kutaka kuirejesha nchi kwenye mstari.

Rais amesema hayo jana alipozungumza na waumini kwenye misa ya Jumapili, katika Kanisa Katoliki parokia ya Tokeo la Bwana Burka jijini Arusha,kwa kusisitiza kumuombea na kumuunga mkono kukabiliana na watu katili   ambao walikuwa wanawaibia Watanzania na kuwanyonya wanyonge.

Amesema analazimika kuchukua hatua ya kuwafukuza kazi si kwamba ni katili, bali lengo ni kuwatumikia Watanzania na kuirejesha nchi kwenye mstari.
 
Rais huyo aliyejibatiza “mtumbua majipu”,  amesema Tanzania ni taifa tajiri, hakuna sababu ya wananchi kulalamika kila kona, kwani kuna ardhi ya kutosha, madini ya kila aina, wanyama wa aina mbalimbali ambao baadhi wameanza hadi kupelekwa nje.

 
"Ninapochukua hatua nataka kuweka Tanzania iliyonyooka, mimi tayari nimesema nimejitoa sadaka kwa watanzania hasa wanyonge," alisema.

KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI