MWANAFUNZI
AWA MGENI RASMI MAHAFARI YA SEKONDARI.
Na Ali
Lityawi, Kahama.
TAASISI
ya Rocken Hill Academy iliyopo wilayani Kahama, imeandikwa historia ya aina
yake baada ya kufanya mahafari ya Shule zake za Msingi na Sekondari, huku Mgeni
rasmi akiwa kijana aliyesomea Shule hizo na kupata mafanikio Makubwa.
Katika
mahafari hayo ya 22 kwa Shule za Msingi za Rocken Hill Academy na Rocken Hill
Junior, na ya 18 kwa Shule ya Sekondari ya Anderlek Ridges huku Mgeni RASMI
akiwa ni mmoja wa wanafunzi waanzilishi wa Shule hizo.
Mgeni
rasmi Dkt Joseph Charles, daktari wa moyo nchini Urusi, amepongeza maendeleo ya
shule hiyo iliyoanzishwa mwaka 1999 ikiwa na madarasa mawili, huku yeye akiwa
miongoni mwa wanafunzi wa awali, alisema maono, bidii na ujasiri vinaweza
kutimiza ndoto.
"Tunaona
hii leo ni mtu mmoja alikuwa na maono na ujasiri mkubwa sana hivyo
haikuwa rahisi mara nyingi binadamu huanzia chini na mwanzo
unakuwa mgumu kukutana na vikwazo”amesema dkt Charles, ambaye pia mwaka
2006.alikuwa miongoni mwa wanafunzi waanzilishi wa Shule ya Sekondari ya
Anderlek Ridges.
Dkt
Charles amesema, ".... ukiamini kitu na kukiweka kwenye maono na bidii ya
kazi ni lazima ndoto itimie hivyo ninampongeza mkurugenzi kwa kutokata
tamaa na kutimiza ndoto yake ambayo leo tunaishuhudia."
Dkt
Charles amesema, "Wanafunzi kwa elimu waliyopita watabadilisha
maisha kwa kupata maarifa na sio ufaulu wa mitihani
na safari yangu ilianza shule ya msingi Rocken Hill na leo hii
nimefika Urusi kama daktari wa magonjwa ya moyo."
Dkt
Charles amewahasa wanafunzi waendelee kuwasikiliza walimu na kuwa na
bidii ili kuweza kutimiza ndoto zao na eneo la shule sio kufaulu
mitihani bali linawajengea uwezo wa kwenda kufanya kazi na kulitumikia taifa.
Kwa
upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Rocken Hill Academy, Sir Alexander
Kazimil, amewataka vijana kutumia teknolojia ya "akili unde" kama
fursa ya kujiajiri, kuongeza kipato na kubuni maisha bora yenye mafanikio
zaidi.
Sir
Kazimil amesema hayo katika mahafali ya Shule ya Sekondari ya Anderlek Ridges
na Shule za Msingi za Rocken Hill na Rocken Hill Junior zinazomolikiwa na
Taasisi ya Rocken Hill Academy zilizopo Mansipaa ya Kahama mkoani Shinyanga,
akiwataka vijana kuifahamu dunia ya utandawazi yenye ubunifu, ushindani na
fursa nyingi.
Sir
Kazimil amesema dunia ya leo haiwapi nafasi watu dhaifu, wasiojotambua,
wazembe, wasio na ndoto wala bidii, hivyo vijana wanapaswa kushindana kimataifa
na kutumia ubunifu kujenga maisha yao yenye mafanikio ya kudumu.
Akieleza
safari yake, Sir Kazimil amesema alianza shughuli kadhaa za ujasiriamali huku
akifundisha shuleni, akisisitiza vijana waanzie chini, waweke maono
mbele, wafanye bidii na kutumia akili unde kwa maadili na kuepuka tabia potofu.
Alisisitiza
ili ufanikiwe ni budi kuwajibika kwa bidii huku ukilipenda jukumu unaloshughulika
nalo na kukuingizia kipato halali na kutokata tamaa, kwani safari ya mafanikio
kuna nyakati huwa na vikwazo.







