WABUNGE wa Majimbo ya
Kawe na Bunda,kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo ( CHADEMA );Halima
Mdee na Esther Bulaya wamehukumiwa kutohudhuria vikao
vyote vya bunge
linaloendelea mpaka mkutano ujao wa Bunge la Bajeti ya 2018/19.Wabunge hao;Mdee wa Jimbo la Kawe na mwezake Bulaya wa Jimbo la Kawe,wamehukumiwa na Kamati ya Maadili,katika Hukumu iliyoungwa mkono na wabunge wengi, waliopitisha azimio hilo kwa kauli ya Kura ya Ndiyooo.
Kamati hiyo ilidai Bulaya na Mdee wamemaliza adhabu za
kawaida zilizopo kwenye kanuni za bunge,ndio maana wameona ni vyema watoe
hukumu hiyo.
Mwenyekiti wa kamati hiyo, George Mkuchika aliliomba Bunge kujadili adhabu inayostahili kulingana na makosa yao.
Kanuni inasema, mbunge anayefanya kosa la kwanza anaweza akazuiwa kuhudhuria vikao visivyozidi 10 na atayakosea kwa mara ya pili anaweza kuzuiwa kuhudhuria vikao visivyozidi 20.
KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI
Mwenyekiti wa kamati hiyo, George Mkuchika aliliomba Bunge kujadili adhabu inayostahili kulingana na makosa yao.
Kanuni inasema, mbunge anayefanya kosa la kwanza anaweza akazuiwa kuhudhuria vikao visivyozidi 10 na atayakosea kwa mara ya pili anaweza kuzuiwa kuhudhuria vikao visivyozidi 20.