Monday, June 5, 2017

MADIWANI SHINYANGA WAHAKIKISHIWA KUSHINDA UCHAGUZI UJAO

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO






SERIKALI Mkoa wa Shinyanga,imewatoa hofu Madiwani katika Halmashauri zilizopo mkoani humo,kuwa hawatarejea katika nafasi zao katika Uchaguzi ujao kwakuwa
itawasimamia,ilimradi wahakikishe wasaidie Serikali iliyopo madrakani kutimiza ahadi zake.

Hivyo katika kutekeleza hayo wameaswa kuondokana na kasumaba ya kulazimisha kuwa na miradi mingi katika Kata zao,bali waelekeze nguvu zao katika kutekeleza miradi michache iliyoibuliwa katika Halmashauri zao.

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga,Zainabu Telack,amesema hayo wakati akiongea na Madiwani wa Halmashauri ya Msalala,wilayani Kahama kwa kuwatoa hofu ya kutochaguliwa Uchaguzi Mkuu Ujao,badala yake wafanye kazi kwa maslahi ya Halmashauri zao na Serikali iliyopo madarakani.

Mkuu huyo wa Mkoa aliwataka Madiwani katika Halmashauri hizo kuondokana na tabia ya kulazimisha Kata zao kuwa na miradi mingi kwa kigezo itakuwa mkombozi kwao katika Uchaguzi ujao,hatua inayosababisha kuchelewesha maendeleo ya Halmashauri husika kutokana na kutokamilika kwa wakati kwa miradi hiyo.

Alisema kuwepo kwa miradi mingi huku mapato yakishindwa kukidhi kuikamilisha imekuwa kigezo cha Halmashauri nyingi kuonekana hazijafikisha maendeleo kwa wananchi,na kusababisha serikali ihukumiwe hivyo kuwataka Madiwani wabadirike kwa kuwa na mradi mmoja katika kila Kata ambayo itakamilika na kuleta tawsira ya maendeleo kwa wananchi wao.

Aliwataka katika kuonesha wanafanya kazi kwa maslahi ya Halmashauri zao,ni vyema pesa zinazopatikana zikawekwa kipaumbele kukamilisha mradi muhimu kwa Halmashauri zao,kwa nguvu zote za Madiwani kuzielekeza hapo na kuepuka  kasumba kuwa miaka mitano itakapopita atahukumiwa iwapo Kata yake,haitokuwa na mradi uliokamilishwa.

“Elekezeni nguvu kwa kuwa wamoja kukamilisha mradi Kata hadi Kata kwa maslahi ya Halmashauri,msihofu kutochaguliwa kisa hujaleta maendeleo katika Kata unayoongoza,tutawasimamia kushinda ilimradi uwe umepigania maendeleo ya Halmashauri yako kwa ujumla.”Alisema Mkuu huyo wa Mkoa.

Aidha aliwataka kushikamana na Watendaji wa Serikali katika kufikisha maendeleo stahiki kwa wananchi huku akiwakumbusha kuwa na utamaduni wa kujibu na kutatua hoja za wananchi pasipo kuzalisha kero zingine.

Kwa upande wake Diwani wa Kata ya Isaka,Dr.Gerald Mwanzia ( CCM ),aliahidi kutoiangusha Serikali ya Awamu ya Tano,kwa kusimamia misingi na miongozo ya watawala ili kufikisha maendeleo stahiki kwa wananchi,huku wakizingatia sera ya Hapa Kazi tu.

Nae Mwenyekiti wa Halmashauri ya Msalala,Mibako Mabubu,alisisitiza kwa madiwani kushikamana na watendaji wa Serikali ili kukamilisha hoja mapema zinazotakiwa na Mkaguzi na Mdhibiti wa Serikali (CAG).

KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI